• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

CCM Yaridhika jengo la Utawala, ICU Geita DC

Posted on: August 25th, 2023

Na Boazi Mazigo- Geita RS

Ziara ya Kamati ya Siasa ya Chama Cha Mapinduzi CCM Mkoa Geita imeendelea ambapo Agosti 25, 2023 kamati hiyo imetembelea miradi mbalimbali ikiwemo jengo la wagonjwa mahtuti (intensive care unit) katika hospitali ya Nzera pamoja na jengo la ofisi ya makao makuu ya Halmashauri na kuonesha kuridhishwa na hatua za utekelezaji miradi hiyo.

Baada ya kupita na kukagua miradi yote, mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Mkoa Geita Nicholaus Kasendamila alisema ameridhishwa kwa namna Halmashauri hiyo inavyosimamia miradi huku akitoa wito kwa Halmashauri zote kuendelea na utaratibu wa usimamizi ulio mzuri kisha kuendelea kumpongeza Mhe.Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyowapambania wana Geita na watanzania kwa ujumla.

"niwapongeze na niwaambie sisi tumeridhika, kazi ni nzuri,hakikisheni mnamaliza kwa wakati ili jengo la makao makuu litumike kama ilivyopangwa na mwanzoni mwa mwezi Oktoba, 2023 tutaangalia kama kweli mmehamia. Pia niendelee kutumia fursa hii kumpongeza na kumshukuru sana Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa namna anavyowapenda wananchi wake, anavyohangaika kutafuta fedha ili kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo, tumuunge mkono, tuisemee miradi"

Mwenyekiti Kasendamila vilevile akiwa kwenye miradi mingine ukiwemo wa Maji Busanda alipokea salamu nyingi za pongezi kwa serikali ya awamu ya sita kutoka kwa Wananchi akiwaomba pia kuendelea kuipokea miradi kuitunza na kuisemea kwa wanajamii wengine wapate kufahamu kazi kubwa inayofanywa na serikali inayoongozwa na CCM.

Akisoma taarifa ya ujenzi wa jengo la wagonjwa mahtuti (intensive care unit), mganga mkuu halmashauri ya wilaya Geita Dkt.Modest Buchard alisema, mradi huo uliletewa shilingi milioni mia tano (shs.500,000,000) ambapo unatarajiwa kukamilika ifikapo Agosti 31, 2023 na tayari wamepokea vifaa tiba mbalimbali kwa ajili ya kuwahudumia wagonjwa mahututi ambavyo baadhi yake vimekwisha kufungwa. Aliongeza kuwa, kukamilika kwa jengo hilo kutaongeza ufanisi wa utolewaji huduma kwa wagonjwa katika mazingira mazuri yenye vifaa bora.

Kamati hiyo imetembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendelea ya sekta ya elimu, maji, maendeleo ya jamii, utawala na afya yenye thamani ya shs.3,725,306,474.95

Ziara ya kamati hiyo itaendelea Agosti 26, 2023 katika Halmashauri ya mji Geita



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa