• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

DC Bukombe Aapishwa, Katibu Tawala Mkoa na DC Geita Wakaribishwa Rasmi Mkoani Geita

Posted on: August 6th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Mhandisi Robert Gabriel, amemuapisha Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mhe. Juma Said Nkumba tarehe 06.08.2018 na kumkaribisha Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita ndugu. Denis I. Bandisa na Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Josephat Maganga ambaye awali alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Bukombe katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Mhe. Mhandisi Gabriel, amewaeleza viongozi wote kwa ujumla wao kuwa yeye amejitolea mawazo, nguvu na akili ili kuiona Geita mpya inayomelemeta, hivyo kuwaonya viongozi kutoshiriki kupokea rushwa ya aina yoyote ile kwani kwa kufanya hivyo Geita mpya itakuwa ni historia tena na kuwaomba wasimwangushe Mhe. Rais kwani wao ndiyo wawakilishi wake kwa wananchi ndani ya mkoa. Akaongeza “nawaomba, nawaomba, naomba sana viongozi msikubali kuchafuliwa na rushwa, tuivunje hiyo laana”.

Baada ya kiapo hicho, Mhe. Said Nkumba amesema “nimepelekwa Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita kufanya kazi na viongozi na siyo makundi ya kisiasa, hivyo wenye makundi ya kisiasa wanipishe nifanye kazi”.

Mhe. Said Nkumba ameongeza kwa kusema kuwa anatambua kuwa Bukombe ni Wilaya ya Kilimo na yenye ardhi nzuri, hivyo atahakikisha anawatumia wataalamu wa kilimo waliyopo ili kuhakikisha ardhi kidogo, inatoa mazao mengi ili kuwanufaisha wananchi.

Kabla ya tukio hilo, Katibu Tawala aliyeteuliwa hivi karibuni ndugu. Denis I. Bandisa alitambulishwa kwa wajumbe na waalikwa waliohudhuria hafla hiyo, kisha akapata nafasi ya kusalimia.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Mbogwe, Mhe. Martha Mkupasi akapata fursa ya kusema neno kwa niaba ya waheshimiwa wakuu wa wilaya wengine ambapo amehimiza ushirikiano baina yao ili kuleta maendeleo ndani ya mkoa ili kuipata Geita mpya.

Baada ya Hafla hiyo, Mkuu wa MKoa wa Geita, Mhe. Mhandisi Gabriel akaendesha kikao cha wadau wa elimu na afya kujadili juu ya mikakati ya kuondokana kabisa na upungufu wa miundombinu ya elimu na afya kabla ama ifikapo juni, 2019. Pamoja na masuala ya elimu na afya, Mkuu wa Mkoa alisisitiza juu ya kuwa na mpango mzuri wa matumizi ya ardhi na kuhimiza juu ya upangaji wa miji na kusema kuwa hatopenda kuona miji mipya ikikuwa pasipo kupangiliwa.

Amesisitiza pia juu ya ukusanyaji wa mapato kwa kuwa lengo la serikali ni Halmashauri kuweza kujitegemea na anaamini baada ya kumaliza changamoto ya upungufu wa miundombinu ya elimu na afya, kasi ya maendeleo itakuwa ni kubwa sana.

Miongoni mwa waliohudhulia hafla hiyo ni pamoja na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wahe.Wabunge, Wenyeviti wa Halmashauri, Wakurugenzi, Wakuu wa Idara na Vitengo,Makatibu Tawala Wilaya, Viongozi wa Dini, viongozi wa Taasisi mbalimbali za Umma na Binafsi, TSN, maafisa habari na waandishi wa habari.




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa