• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Elimu Zaidi Kuhusu Barabara Itolewe – Aagiza RC. Robert Gabriel

Posted on: February 21st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amewaagiza wataalam wa Wakala wa Barabara Tanzania( TANROADS) na Wakala wa Barabara za vijijini na mijini( TARURA) katika mkoa wa Geita kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi wa Mkoa huo juu ya matumizi sahihi na utunzaji wa barabara. Mhandisi Robert Gabriel ameyasema hayo wakati wa kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa wa Geita  kilichoketi tarehe 21/02/2019 katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.


Mhandisi Gabriel ameongeza kuwa uwepo wa barabara nzuri katika Mkoa wake ni jambo la msingi na barabara ni moja ya raslimali adimu inayostahili matunzo hivyo wadau wa barabara wanatakiwa waendelee kuwaelimisha wananchi kutovamia hifadhi za barabara kwa kujenga, kulima, kupitisha mifugo, wizi wa alama za barabani, vyuma na makalavati. Pia kuepuka matumizi yote yasiyo rasmi na yasiyoruhusiwa.

Mhandisi Robert Gabriel amesema kuwa barabara ni uchumi na maendeleo kwani  mazao, bidhaa mbalimbali za kibiashara husafirishwa kutoka eneo moja hadi jingine, zikitunzwa vizuri zinaondoa umaskini. Pia barabara imara inapokuwepo inasaidia kuokoa maisha ya wagonjwa na kina mama wajawazito kwa kuwawahisha katika vituo vya huduma za afya pindi inapohitajika.

Mkuu wa Mkoa wa Geita  ametumia fursa hiyo pia kuwataka wataalam wa Wakala wa barabara kwa kushirikiana na wakurugenzi wa Halmashauri zote za Mkoa wa Geita kufuatilia na kusimamia kwa karibu miradi inayotekelezwa ili kupata miradi yenye ubora wa hali ya juu na gharama ya miradi iendane na utekelezaji halisi.

“Mamlaka za barabara hakikisheni kazi za ujenzi na ukarabati wa barabara zinazotolewa kwa wakandarasi  wawe ni wenye weledi, uadilifu, uzoefu na uwezo wa mitambo yenye ubora. Ni aibu kwa Mkoa wa Geita kumpa kazi ya ujenzi wa barabara aliyeharibu kazi katika mikoa mingine hivyo mnatakiwa kufanya utafiti wa kina kabla ya kuajiri mkandarasi yeyote.” Aliongeza Mhandisi Robert Gabriel.

Kwa upande wake Meneja wa Wakala wa Barabara Tanzania Mkoa wa Geita Mhandisi Harun Senkuku amesema kuwa licha ya jitihada zinazofanywa na Serikali katika kuhakikisha barabara zinatengenezwa bado wanakabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya dhamira mbaya ya baadhi ya wasafirishaji kupitisha mizigo mizito kwenye barabara kinyume na matakwa, sheria na kanuni za barabara.

Mratibu wa Wakala wa Barabara za vijijini na mijini( TARURA) wa Mkoa wa Geita Mhandisi Gaston Paschal amesema TARURA imejipanga kuwajengea uwezo wakandarasi wazawa ili waweze kufanya kazi zenye ufanisi. Pia kutoa elimu kwa wananchi kupitia mikutano ya watendaji wa Serikali na wanasiasa juu ya utunzaji wa barabara kwa mujibu wa sheria ya barabara yam waka 2007.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale ambaye ni mjumbe wa Bodi ya barabara ametoa ushauri kwa Wakala wa barabara vijijini na mijini( TARURA) kutenga fedha katika bajeti zao kwa ajili ya ukarabati wa barabara wa dharura pindi inapotokea barabara zimekatika hususani wakati wa kipindi cha masika.

Kwa Mwaka wa fedha 2018/2019 jumla ya shilingi Bilioni 3.28 za kitanzania zimetengwa kwa ajili ya miradi midogo ya maendeleo ya ukarabati wa barabara za Mkoa na Halmashauri za Wilaya katika Mkoa wa Geita




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa