• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Geita ni Dhahabu, Tutashirikiana Kuleta Matokeo, Asema Bi. Natalie BOUCLY wa UNDP

Posted on: January 20th, 2019

Ni majira ya saa nne asubuhi ya tarehe 20.01.2019, ujumbe wa Bi.Natalie BOUCLY, Mkurugenzi Mkazi wa UNDP Tanzania unawasili na kupokelewa Mkoani Geita na mwenyeji wao Mhe. Mhandisi Robert Gabriel, Mkuu wa Mkoa wa Geita kisha kufanya mazungumzo yenye lengo kuu la ushirikiano katika maeneo mbalimbali ya uwekezaji.

Akiukaribisha ujumbe huo, Mhe. Mhandisi Gabriel amemweleza Bi. Natalie juu ya namna ambavyo mkoa umejipanga kuwa na Geita mpya huku akiitaja miradi ya kimkakati itakayotekelezwa kwa mwaka huu 2019, itakayobadili taswira ya mkoa na kuufanya uwe wa kiuwekezaji na kuinuka kiuchumi.

Amesema, “Geita tunahitaji matokeo kwenye miradi, tungependa tuungane nanyi UNDP katika kuhakikisha tunafungua ukanda wa uwekezaji na utalii Geita, tuwe na kijiji cha utalii, lakini vilevile tuwe na utalii wa asili, tuwakaribishe wageni kujifunza mila na desturi (tamaduni) za jamii ya Geita. Jambo jingine ni kuandaa soko maalumu kwaajili ya wachimbaji wadogo wadogo kuweza kuuza dhahabu yao huku wakipata teknolojia bora ya uchakataji na uchenjuaji madini hayo bila kusahau kuitangaza Rubondo kama hifadhi inayopatikana Geita yenye vivutio vingi”.

Naye Mkurugenzi Mkazi wa UNDP Tanzania Bi. Natalie BOUCLY aliyeambatana na Bw. Amon Manyama, Mratibu wa Miradi UNDP na Bw. Joshua Mirumbe ambaye ni Mshauri, alionesha kufurahishwa na mapokezi aliyoyapata kutoka kwa mwenyeji wake huku akisema “nimefurahi sana, sijasemeshwa Kifaransa tangu nimekuwa nikizunguka” kisha kueleza jinsi UNDP inavyofanya kazi zake nchini ikiwemo uhifadhi wa misitu asilia.

Bi Natalie amesema, “kwa Geita tutaangalia namna ya kushirikisha Kampuni ya Africa Mining Vision na UNDP Ghana ili kuweza kufanikisha suala la namna nzuri ya kusaidia soko la dhahabu ya wachimbaji wadogo wadogo Geita, kwakuwa tunao wataalam katika eneo hili, lakini vilevile kupitia mradi tunaoendelea nao wa utunzaji misitu asilia, tutaweza kuitangaza Hifadhi ya Rubondo, na tunawapongeza kwa utajiri uliyopo Geita, Geita ni Dhahabu”.


Katika mazungumzo hayo, Bi. Natalie aliongeza kusema kuwa, ni vyema kushirikisha nchi jirani zenye shughuli za kitalii ili katika safari zao, Geita iwe ni sehemu ya utalii kwani watalii wengi hupenda hata kuangalia mashamba ya mazao kama yanayopatikana Geita ikiwemo Nanasi, Pamba, Muhogo, uchimaji mdogo mdogo na hatua za upatikanaji wa dhahabu n.k na kwamba hata katika mikutano watakayokuwa wakiendesha wanapokuwa na wafadhili mbalimbali, basi watakuwa mabalozi wazuri wa kuitangaza Geita na vivutio vyake ikiwemo Kisiwa cha Rubondo.

UNDP Tanzania kupitia uwakilishi wake, wamesema wataendelea kuwa na ushirikiano na Geita katika utekelezaji wa miradi mbalimbali, hivyo wafurahia uwepo wao Mkoani Geita kutokana na namna mkoa ulivyojipanga kuinua maisha ya wananchi wake.

Miongoni mwa waliyoshiriki katika mazungumzo hayo ni Baadhi ya Wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Josephat Maganga, Mkurugenzi wa Mji Geita Eng. Modest Aporinary na Meneja wa SIDO Mkoa wa Geita Bw. Japhary Donge.

Kwa hakika, Geita mpya inakuja kutokana na ndoto na maono mengi aliyonayo Mkuu wa Mkoa Mhandisi Gabriel, na katika mikutano yake amekuwa akimwomba Mungu ili mazuri mengi anayoyapanga kwaajili ya Geita yatimie na mara nyingi amekuwa akisema “tulichelewa sana, Geita ni tajiri, hivyo ni lazima mkoa ufanane na utajiri ulionao, wananchi pia wanufaike na utajiri wa mkoa huu”.

Hivyobasi, Watanzania mnaendelea kukaribishwa mkoani humu, mkoa wa kiuwekezaji, hakuna urasimu, rushwa wala ubadhilifu “kwetu ni zilipendwa”, mazingira sahihi na rafiki kwa uwekezaji.

Geita: Amani, Umoja na Kazi




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa