• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Geita Yapunguza Maambukizi ya VVU

Posted on: December 4th, 2024


Hali ya Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI katika Mkoa wa Geita imeshuka kwa asilimia 4.9% ikiwa yamepungua kwa asilimia 0.1% kutoka wastani wa mwaka 2016/17 ambapo maambukizi yalikuwa 5.0%

Takwimu hizo zimebainishwa na Mratibu wa UKIMWI Mkoa wa Geita Dkt. Yohane Kihaga hivi karibuni wakati wa Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani yaliyofanyika kimkoa katika kata ya Bukwimba Wilaya ya Nyang’hwale.

Dkt. Kihaga ameeleza kuwa Mkoa wa Geita unakadiriwa kuwa na watu 95,100 wanaoishi na virusi vya UKIMWI kati ya watu hao asilimia 73.1 wanatambua hali ya maambukizi ya VVU, na asilimia 98.4 ya hao wanatambua hali zao na wanatumia dawa za kufubaza virusi vya UKIMWI, huku asilimia 98.8 wakiwa tayari wamefubaza VVU.

Mratibu wa UKIMWI Mkoa wa Geita amebainisha mazingira yanayochochea mwendelezo wa maambukizi ya Virusi vya UKIMWI katika Mkoa wake ni pamoja na hekaheka za mapambano ya maisha ikijumuisha maeneo ya uchimbaji mdogo wa dhahabu, uvuvi, minada, maegesho makubwa ya malori, vilabu vya pombe za asili na ujenzi wa miradi mikubwa kama Bomba la mafuta kutoka Hoima Uganda.


Dkt. Kihaga amebainisha kuwa Mkoa wa Geita umelenga kushirikiana na wadau kuhakikisha wanapambana na tatizo la Maambukizi ya Virusi vya UKIMWI kwa kuendelea kutoa elimu juu ya tahadhari dhidi ya maambukizi mapya ya VVU kwa kutumia njia rafiki watakazozibuni pamoja na kufanya upimaji wa VVU kwa kuwafuata watu kwenye maeneo maalum wanayoishi au kufanyia shughuli.

Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Geita ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Geita Mheshimiwa Hashim Komba ametoa rai kwa vijana na wanaume kujenga utamaduni wa kupima afya zao ili kujitambua na sio kutegemea majibu yanayopatikana baada ya wake zao kupimwa kipindi cha ujauzito.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita ASCP Safia Jongo ametoa wito kwa jamii kuhakikisha wanawalinda watoto dhidi ya vitendo vya ukatili pamoja na kuwakinga dhidi ya maambukizi ya Virusi vya UKIMWI ili waweze kutimiza malengo yao katika maisha.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake wanaoishi na Virusi vya UKIMWI, Ndg. Ponsian Magezi ametoa wito kwa Serikali kuendelea kutoa elimu kwa jamii ili watu wanaoishi na maambukizi ya VVU wasinyanyapaliwe wala kutengwa katika jamii.

Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI Duniani hufanyika kila mwaka kwa lengo la kuikumbusha jamii juu ya uwepo wa janga la UKIMWI na athari zake ili kuweza kuchukua tahadhari za kujilinda. Kwa mwaka 2024 Maadhimisho hayo yameongozwa na Kauli Mbiu isemayo"CHAGUA NJIA SAHIHI, TOKOMEZA UKIMWI".

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa