• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

GEITA Yawaapisha Wasimamizi 6 wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa

Posted on: September 12th, 2019

Kama ilivyo kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Na.292 Marekebisho ya Mwaka 2015 Kifungu cha 9(5), ambacho kinamtaka kila Msimamizi wa Uchaguzi na Msimamizi Msaidizi wa Uchaguzi kuapa viapo vya Uaminifu, Utii na Uadilifu Mbele ya Hakimu baada ya kuteuliwa, mkoa wa Geita umetekeleza sheria hiyo kwa kuwaapisha jumla ya wasimamizi wa uchaguzi wa serikali za mitaa sita (6) kutoka halmashauri sita za zinazounda mkoa huu walioambatana na maafisa uchaguzi kutoka kwenye halmashauri hizo.

Akizungumza ofisini kwake kabla ya tukio la kuapishwa wateule hao lililofanyika Septemba 12, 2019, Katibu Tawala Mkoa wa Geita Bw. Denis Bandisa amesema, wasimamizi wa uchaguzi walioteuliwa wanapaswa kuzingatia kuwa uchaguzi kwa mwaka huu umepangwa kufanyika Novemba 24, 2019 na hivyo wanapaswa kutambua yakuwa, kiapo walichokula ndicho kitawafanya wafanye kazi hiyo vizuri na watawajibika kwacho iwapo hawatafanya vizuri.

“pamoja na kutambua wajibu wenu kupitia kiapo mlichokula, ambacho kimewapa uhalali wa kufanya majukumu yenu yakiwemo ya kutoa tangazo la majina ya vijiji, mitaa na vitongoji kwa wakazi wa maeneo hayo kwa kuzingatia orodha ya vijiji, vitongoji na mitaa kama ambavyo yametolewa kwenye tangazo la serikali, mnatakiwa kuhakikisha kesho mnatangaza maeneo haya ya uchaguzi ikiwa ni jukumu lenu la kwanza kulitekeleza, hivyo ninaamini mtatekeleza majukumu yenu kwa haki na uadilifu”, amesema Bandisa.

Bw. Bandisa amemaliza kwa kuwasisitiza wasimamizi hao wa uchaguzi akiwaambia kuwa wanatakiwa kutambua kwamba, wao ndiyo watakuwa wasemaji wa kutoa maelezo na maelekezo mbalimbali kuhusiana na uchaguzi utakaofanyika, lakini pia wataunganisha ratiba za kampeni kutoka kwa vyama mbalimbali vya siasa kwa kushirikiana na mkuu wa polisi wilaya (OCD) ili kuepusha migongano na miingiliano wakati wa kampeni na mwisho kuunganisha taarifa ya matokeo ya uchaguzi na kuweka kumbukumbu.

Naye Hakimu Mkazi Mfawidhi Wilaya ya Geita Mhe.Gabriel Nimrod Kurwijila kabla ya kuwaapisha walioteuliwa amewaambia kuwa, wanapaswa kutambua yakwamba, kwa sasa wanaajiriwa kwa kazi ya kusimamia uchaguzi kutoka kwa mwajiri wao ambaye ni waziri mwenye dhamana na uchaguzi wa serikali za mitaa, hivyo kazi hiyo ikafanyike kwa kadiri ya viapo watakavyoapa, kisha kuwaapisha tayari kwa kuanza kazi.

Kwa upande wake Bi.Sania Mwangakala ambaye ni Mratibu wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita, amewapongeza wasimamizi hao kwa kuteuliwa na kusema lengo la kukutana hapo ni wao kuapa ili kuwa huru kuanza kutekeleza majukumu yao.

Jumla ya Mitaa 65, Vijiji 486 na Vitongoji 2,195 vitashiriki katika wa Serikali za Mitaa Novemba 24, 2019


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa