• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Halmashauri za Mkoa wa Geita Zasisitizwa Kutenga Fedha Kwaajili ya Shughuli za Lishe.

Posted on: January 19th, 2019

Hayo yamejiri wakati wa Kikao cha Kamati Jumuishi ya Lishe Mkoa wa Geita kilichofanyika tarehe 19.01.2019 katika ofisi ya Mganga Mkuu, Mkoa wa Geita

Akiongea kabla ya kuweka kikao wazi, Mwenyekiti wa Kamati  na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Geita Bw.Herman Matemu amesema kuwa, taarifa zinaonesha kuwa bado mkoa wa Geita haujafanya vizuri katika suala zima la lishe, hivyo kusema kuwa kamati inatakiwa kuwajibika kwa kushauri ipasavyo kupitia taarifa zao na mwisho wa siku watendaji kutekeleza vizuri ili kuinua asilimia ya lishe bora ndani ya mkoa.

Amesema, “kama kamati tunao wajibu wa kufanikisha suala zima la lishe kila mmoja katika kila eneo lake na kusema hata kuwa, kwenye eneo la kilimo twapaswa kuwaelimisha wananchi ili walime mazao mchanganyiko yatakayowawezesha kupata mazao yenye kuwapatia lishe iliyo bora na kusisitiza kuwa bado upo umuhimu wa kuwakutanisha wadau wanaoshughulika na lishe ndani ya mkoa, wawasilishe mipango yao ili kuepusha migongano katika utekelezaji wake bila kusahau kuwa Halmashauri zote zinatakiwa kuendelea kuweka na kutenga kwenye bajeti fedha kwaajili ya lishe.”

Katika kikao hicho, wajumbe wamekumbushwa kuhakikisha wanawasilisha mpango mkakati wa kila sekta wa namna shughuli za lishe zitakavyokuwa zikitekelezwa kwenye kikao kijacho, ambapo awali shughuli za lishe zilitekelezwa na watumishi wa afya kwa kiwango kikubwa.

Halmashauri bado zinaelekezwa kuendelea kutenga fedha kwa ajili ya shughuili za lishe ili zisikwame wakitambua kuwa, serikali imetilia mkazo suala hilo kwamba ni muhimu sana kuzingatia, huku Ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa kupitia Mganga Mkuu wa Mkoa Dkt. Japhet Simeo ikiahidi kuwa,hadi kufikia mwezi machi, 2019 wanatarajia kuanzisha utaratibu wa kutengeneza chakula dawa japokuwa tayari wameweka kwenye bajeti ununuzi wa chakula dawa cha kisasa kupita bohari ya dawa MSD.

Nao wajumbe wakiwemo wadau wa lishe Mkoa wa Geita wameahidi kukutana wakati utakapofika ili kwa pamoja waje na mpango utakaorahisisha utekelezaji na isiwe kama awali ambapo kuna mahala wamejikuta wakitekeleza shughuli moja ilihali wadau ni tofauti

Awali afisa Afya Mkoa Bi. Tibezuka John aliwaeleza wajumbe kuwa, hadi robo ya pili yaani mwezi Oktoba hadi Desemba 2018, shughuli mbalimbali zimetekelezwa zikiwemo usimamizi na ufuatiliaji shirikishi, vikao vya kamati jumuishi vya lishe, kutembelea kaya na kutoa elimu ya ufahamu kwa lengo la kupunguza udumavu n.k



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa