• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kampuni ya GGM Yatakiwa Kutoa Kazi Za Huduma Kwa Wakazi wa Geita

Posted on: February 20th, 2018

Kampuni Ya GGM Yatakiwa Kutoa Kazi Za Huduma Kwa Wakazi Wa Geita

Mkuu wa Mkoa wa Geita na Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama  Mhandisi Robert Gabriel Luhumbi ameutaka Uongozi wa Kampuni ya Uchimbaji wa Madini ya Geita (GGML) kutoa fursa za utoaji wa huduma katika mgodi huo kwa vikundi mbalimbali vya Ujasiriamali vilivyoko Mkoani Geita.

Agizo hilo limetolewa hivi karibuni wakati Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Geita ilipotembelea Mgodi huo kwa lengo la kukagua na kuona namna unavyoendesha shughuli zake za kila siku.

Mhandisi Robert alitaja fursa ambazo vikundi vya ujasiriamali vya Wanawake na Vijana vinavyojishughulisha na kilimo pamoja na ufugaji katika Halmashauri za Mkoa wa Geita vinaweza kuuza bidhaa zao kwa kampuni ya GGM kama vile kuuza vitoweo vya kuku, nyama ya ng'ombe, kondoo, sungura, matunda na Mchele tofauti na hivi sasa ambapo bidhaa hizo huagizwa nje ya Mkoa wa Geita.

''Ili kukuza uchumi wa wananchi na Mkoa kuna umuhimu wa Kampuni kutoa fursa kwa vikundi vyetu ili vianze kutoa huduma kwa sababu Halmashauri za Mkoa kupitia mfuko wa wanawake na vijana wako tayari kuvikopesha mitaji vikundi hivyo ili viwe na nguvu ya kutoa huduma hizo kwa kampuni''. Aliongeza Mkuu wa Mkoa.

Aidha, aliagiza kuwa fedha ya huduma ya jamii (CSR) inayotolewa na Mgodi kwa Mkoa wa Geita lazima ifahamike kwa Umma na namna inavyotumika ili kuwa na uwazi kati ya Kampuni, Serikali na jamii inayozunguka mgodi wa GGM. Pia, aliwataka viongozi wa mgodi kuwachukulia hatua za kisheria na kuwawajibisha watumishi wao watakaobainika kutumia nafasi zao kwa maslahi binafsi.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Mgodi wa GGM Ndugu Richard Jordinson aliishukuru kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa kwa Kutembelea mgodi na kujionea shughuli zinazofanyika na kuahidi kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Mkuu wa Mkoa.

Vile vile alieleza kuwa kuwa kampuni ya GGM itaendelea kushirikiana na jamii katika shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii.

Katika Ziara hiyo kamati ya Ulinzi na Usalama ilipata fursa ya kutembelea mgodi wa chini na juu pamoja na eneo la uzalishaji (Process Plant).

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa