• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC GEITA: Nyang'hwale Mnaenda vizuri, hongereni sana.

Posted on: December 10th, 2021

Leo Desemba 10, 2021 Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Rosemary Senyamule amefanya ziara kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale kukagua Utekelezaji wa Ujenzi wa Miradi ya Ujenzi wa Madarasa kwa fedha za Mpango wa Maendeleo kwa  Ustawi wa Taifa na Mapambano Dhidi ya Uviko 19.

Mhe. Mkuu wa Mkoa amewapongeza viongozi wa Halmashauri hiyo kwa usimamizi mzuri wa miradi ya Ujenzi wa Madarasa kwani kwa wastani shule zote wametekeleza kwa zaidi ya 83% na kwamba hadi kufikia Desemba 15, 2021 wana mikakati kukamilisha hadi kuweka Samani kwenye madarasa.

"Tuna kitu cha kujifunza kutoka kwenye Shule hii maana kwenye maeneo mengine sijaona Miundombinu ya walemavu kuingilia kwenye madarasa lakini hapa nimeona leo, na nawasihi wengine waliodhani wataweka mwishoni wasije wakasahau jambo hili muhimu," amesema Mhe. Mkuu wa Mkoa akikagua ujenzi kwenye shule ya Sekondari Izunya.

Wakati huohuo, Mkuu wa Mkoa ameonesha furaha yake kwa Utekelezaji mzuri wa miradi ya Ujenzi wa Vituo vya Afya kutoka Fedha za Tozo kwani Halmashauri hiyo imetekeleza kwa kasi na viwango bora na amezitaka Halmashauri zingine kuiga mfano huo na kuhakikisha ifikapo Desemba 31, 2021 wakamilishe vituo hivyo.

 "Kingine cha kuwapongeza Nyang'hwale ni ujenzi wa miradi ya Vituo vya Afya kutoka kwenye Fedha za Tozo, pamoja na ujenzi wa Madarasa nyie mmeonesha kuwa Miradi ya Serikali inaenda kwa pamoja hivyo na Halmashauri zingine ambao wamekua wazito naomba wajifunze hapa," amesema.

"Idara ya Elimu Sekondari ilipokea jumla ya Tshs. Milioni 800 kwa ajili ya Ujenzi wa vyumba vya madarasa 40 na Tshs. Milioni 280 kwa ajili ya vyumba vya madarasa 14 katika shule za Msingi Nne Shikizi." Amesema Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Mhe. Jamhuri Wiliam.

Aidha, Mhe. Mkuu wa Wilaya amebainisha changamoto ya samani na milango kupatikama kwa shida kidogo lakini amesema  wanatarajia kuzitatua na kwenda na wakati."Changamoto tuliyonayo Mhe. Mkuu wa Mkoa ni madawati na kasi ya utengenezaji wa milango tumeona siyo nzuri sana ila tunaendelea kufuatilia kwa karibu ili tuweze kukamilisha kwa wakati."

"Mhe. Mkuu wa Mkoa,  shule hii ilipokea Tshs. Milioni 60 kwa ajili ya Ujenzi wa vyumba vya Madarsasa 3, Mradi huu utapunguza Utoro kwa wanafunzi na utaongeza wataalamu nchini kwa faida ya Taifa letu" Mwalimu Deogratiana Mwangalaba, Mkuu wa Shule Izunya Sekondari.

Mhe. Mkuu wa Mkoa shule ya Sekondari Msalala tulipokea Tshs. Milioni 80 kwa ajili ya ujenzi wa Vyumba 4 vya madarasa lakini tunatekeleza Ujenzi wa vyumba 4 vya Madarasa na Ofisi Moja kwa ubora unaokusudiwa kwa Tahs. Milioni 80 hiyohiyo na tutabakisha na kiasi kidogo cha Fedha." Mpuya Mlyakado, Mkuu wa Shule ya Msalala.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa