• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mafunzo Kazini Yasisitizwa kwa Waajiri Geita

Posted on: May 1st, 2023

Na Boazi Mazigo - Geita

Mkuu wa mkoa geita Mhe.Martine Shigela ametoa rai kwa waajiri wote mkoani geita kuzingatia suala la mafunzo kwa wafanyakazi ikiwa ni sehemu ya kuboresha maslahi na mazingira bora kwa mfanyakazi ili kuongeza tija na ufanisi kwenye taasisi, shirika au kampuni.

Rai hiyo imetolewa Mei Mosi, 2023 wakati akizungumza na wafanyakazi kutoka taasisi za umma na binafsi mkoani Geita baada ya kupokea maandamano yao wakati wa maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani Mei Mosi ambapo kwa mkoa wa geita imeadhimishwa katika uwanja wa CCM Kalangalala na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali.

RC Shigela alisema, serikali inayoongozwa na Mhe.Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan inawajali wafanyakazi na ndiyo maana imeendelea kuboresha maslahi yao na kwamba, ili taasisi ziweze kukabiliana na changamoto mpya za kimaendeleo katika utendaji, ni vyema waajiri kuzingatia kuwapa mafunzo wafanyakazi wake kama sehemu ya kuongeza ufanisi na kuwataka waajiri ambao hawajaanza kutekeleza maelekezo ya serikali ya kima cha chini cha mshahara kufanya hivyo mara moja.

“viongozi, ni vyema muwajengee uwezo wafanyakazi walio chini yenu, kuna mabadiliko duniani, hivyo ni muhimu kuwa na bajeti zinazojumuisha watenda kazi kupata mafunzo wawapo kazini. Mbali na hilo, niwaombe waajiri kujenga mazingira mazuri kwa wafanyakazi kwani ni vizuri kumfanya huyu mfanyakazi ajihisi ni sehemu ya taasisi kwa jinsi unavyomtendea na kumjali” alisema RC Shigela.’

Pamoja na kusema hayo, RC Shigela alihimiza juu ya haki na wajibu kwa pande mbili kati ya muajiri na muajiriwa akimaanisha kuwa, wafanyakazi nao wana wajibu wa kufanya kazi kwa weledi na ubunifu ili kuongeza ufanisi katika taasisi na kwamba kwa hali hiyo, kama kila mmoja akifanya sehemu yake basi maslahi nayo yataendelea kuboreshwa. Pia alisisitiza juu ya wafanyakazi kutofanyishwa kazi sizizo na staha, kuzingatia utu na taratibu katika kuwajibishana pale inapotokea changamoto kwa mfanyakazi kama ambavyo katiba ya nchi inavyothamini utu, na mwisho akagawa vyeti vya watumishi hodari pamoja na zawadi kwa washindi wa michezo mbalimbali.

Awali akizungumza kwaniaba ya Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi TUCTA Geita, katibu wa TAMICO Bw.Obed Mwakapango alisema bado ziko changamoto mbalimbali zinazowakabili watumishi ikiwemo malimbikizo, taasisi binafsi kutozingatia viwango vipya vya mishahara, baadhi ya waajiri kutopeleka michango kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii n.k na kuiomba serikali kuingilia kati suala hilo ili kuendelea kuboresha maslahi ya mtumishi

Naye katibu tawala mkoa Geita Prof.Godius Kahyarara alisema, “ndani ya miaka miwili ya uongozi wa Mhe.Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan, mengi yamefanyika kwa watumishi hivyo hatuna budi kumshukuru. Kama mkoa tunasisitiza juu ya ajira zenye staha, lakini tuhakikishe tunawajibika ipasavyo na kutimiza wajibu ili iendane na kudai maslahi”. Alimaliza kisha kuwapongeza wafanyakazi walioshiriki siku hiyo adhimu.

Kwaniaba ya CCM Mkoa Geita, Bi Mary Mazula aliwapongeza watumishi wote akiwasifu kwa utendaji kazi na kutoa wito kwa sekta binafsi kuhakikisha zinazingatia maelekezo ya kima cha chini cha mshahara na kwamba kama chama tawala ni wasikivu na wataendelea kupambania haki na stahiki za wafanyakazi.


“Hakika Mishahara Bora na Ajira za Staha ni Nguzo kwa Maendeleo ya Wafanyakazi, na Mhe.Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan, Amethibitisha”



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa