• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Maji Hayana Mbadala, Tutunze Chanzo cha Mto Nikonga”. Asema RC Geita

Posted on: June 26th, 2022

Mkuu wa mkoa wa Geita Mhe.Rosemay Senyamule amezindua uhifadhi na utunzaji Mto Nikonga ikiwa ni jitihada za serikali kupitia bodi ya maji ya bonde la ziwa Tanganyika chini ya wizara ya maji kuhifadhi vyanzo vya maji nchini.

Uzinduzi na uhifadhi huo umefanyika Juni 25, 2022 katika kata na kijiji cha kamena ulipo Mto Nikonga ndani ya halmashauri na wilaya ya Geita, mto ambao ni miongoni mwa kidakio cha mto Malagarasi, huku mkuu wa mkoa huyo akisisitiza juu ya wananchi kutekeleza sheria ya uhifadhi vyanzo vya maji, kutunza vyanzo vya maji na kwamba ni muhimu wananchi kutambua kuwa maji ni rasilimali adimu waitunze.

Akiongea wakati wa uzinduzi huo RC Senyamule alisema “maji ni rasilimali isiyo na mbadala, tutunze vyanzo vyetu kwa pamoja. Tuwe pamoja na si mmoja mmoja kwenye hili. Kumekuwa na upungufu wa maji kwakuwa vyanzo vingi vinaharibiwa, hivyo tushikamane kuhifadhi chanzo hiki” .

Aliongeza kwa kuiagiza Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) mkoa wa Geita kuhakikisha wanapanda miti rafiki wa maji kwa kushirikiana na uongozi wa kamena na baadaye kuwakumbusha wananchi wa kamena kuhakikisha hawafanyi shughuli za kibinadamu ndani ya mita sitini (60) kama ilivyoelezwa kwenye sheria kisha kutembelea chanzo na kuzindua uhifadhi kwa kusimika bango na nguzo.

RC Senyamule alimaliza kwa kuwakumbusha wananchi kujiandaa kuhesabiwa pale zoezi la sensa ya watu na makazi litakapoanza ifikapo agosti 23, 2022 pamoja na kujiandaa kushiriki kwenye mbio za mwenge wa Uhuru kwa mwaka huu ambapo kwa mkoa wa Geita zinatarajiwa kuanza Julai 20, 2022

Awali akisoma taarifa ya mradi, mwakilishi wa mkurugenzi wa bonde la ziwa Tanganyika mhandisi Odemba Cornel alisema, Mto Nikonga ni mojawapo ya kidakio kidogo cha mto Maragarasi na kwamba mto huo ni miongoni mwa mito inayokabiliwa na uchafuzi wa mazingira na maji kwa kiasi kikubwa kutokana na shughuli za kibinadamu zinazofanywa ndani ya mita 60 ambazo ni hifadhi ya mto kwa mujibu wa sheria ya mazingira fungu la 57 na sheria ya rasilimali za maji namba11 ya mwaka 2009 kifungu cha 34 na kwamba mradi huo ulitengewa kiasi cha Milioni 420 ili kuhifadhi na kuutunza mto huu na matawi yake kuanzia kijiji cha Kamena hadi pori la Bukombe/Ushirombo ambao una urefu wa takribani km 55.

Mhandisi Odemba aliongeza kuwa, miongoni mwa faida za mto Nikonga  ni pamoja na kuwa ni mto pekee unaotegemewa na wakaazi zaidi ya 70,000 waishio kandokando ya mto huo kwa mujibu wa taarifa ya kijiji na ni mto unaotengeneza ikolojia inayopendeza hasa katika maeneo ya hifadhi kama misitu ya Rwamgasa, Ushirombo na Kigosi na kwamba mto huu huchangia kiasi kingi cha maji katika mto Moyowosi, Malagarasi na Ziwa Tanganyika.

Aidha, mhandisi Odemba alihitimisha kuwa “pamoja na umuhimu wa mito hii kwa jamii yetu, bado inakabiliwa na changamoto kama matumizi holela kwa shughuli za uchenjuaji madini, kilimo na ufugaji, uzuiaji wa mto (ili kuvua samaki) hali ambayo huondoa uwiano wa matumizi ya maji baina ya watumiaji, upungufu wa maji, maji kujaa matope n.k”.

Nao Mhe.Alhaj Said Kalidushi ambaye ni mwekiti wa CCM mkoa wa Geita, Mhe.Wilson Shimo, DC Geita na Mhe.Peter Ndekela, diwani wa Kamena kwa nyakati tofauti waliwasihi wananchi kutekeleza shughuli hiyo na kwamba baada ya uzinduzi huo kamati ya usalama wilaya itakuwa ikipita kuhakikisha hakuna shughuli mpya inaanzishwa kama kilimo kwenye eneo la hifadhi ili kuendelea kutunza chanzo hicho.

Bonde limepanga kutekeleza uhifadhi na utunzaji kwa kuweka alama kuanzia Kamena hadi Kashishi urefu wa Km 10, ambapo nguzo 400 na mabango 20 vitasimikwa pande zote za mto na pia bonde limeanzisha jumuiya ya mto Nikonga ukanda wa juu.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa