• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mama Samia Legal Aid Yawanufaisha Wananchi 161,151 Geita

Posted on: February 8th, 2025


Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita Ndugu Mohamed Gombati amepokea taarifa ya utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (Mama Samia Legal Aid Campaign) ambayo imewafikia wananchi 161,154 katika Mkoa wa Geita.

Katibu Tawala Mkoa wa Geita ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maono yake ya dhati ya kuleta kampeni hii kwa wananchi kwa lengo la kuwasaidia kupata huduma mbalimbali za kisheria ambazo zimekuwa zikiwatatiza kwa kipindi kirefu pasipo kupatiwa ufumbuzi kwa sababu ya uwezo mdogo wa kifedha kwa wananchi walio wengi kulipia gharama za Mawakili.

“ Kampeni hii imekuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa Mkoa wa Geita kwa sababu imeweza kutatua migogoro ya ardhi na mipaka iliyodumu kwa miaka mingi pamoja na migogoro mingine ya kijamii. Napenda kumshukuru Waziri wa Katiba na Sheria pamoja na wataalam wake kwa kuwaongezea ujuzi wa kazi za utatuzi wa migogoro mbalimbali  Maafisa wa madawati waliopo mkoani kwetu.” Aliongeza Ndg. Mohamed Gombati.


Ndg. Mohamed Gombati ametumia wasaa huo kutoa mwaliko kwa Wizara ya Katiba na Sheria kutumia fursa ya Maonesho ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika Mkoani Geita kila mwaka kwa kushiriki na kuendelea kutoa elimu ya masuala mbalimbali ya kisheria kwa wananchi.

Akiwasilisha taarifa hiyo, Mratibu wa Kampeni kwa Mkoa wa Geita Wakili wa Serikali Bw. Candid Nasua amesema hadi kufikia Februari 4, 2025 walifanikiwa kukamilisha zoezi la Kampeni ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia ambapo wamefika katika Halmashauri zote sita,Kata, Vijiji na Mitaa iliyopangwa na kuwezesha migogoro 86 kutatuliwa papo kwa papo na migogoro 498 inaendelea kushughulikiwa ili kuipatia ufumbuzi.

Kampeni ya Mama Samia Legal Aid iliyofanyika kwa siku tisa iliambatana na utolewaji wa huduma ya usajili wa matukio muhimu ya binadamu iliyotolewa na Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini( RITA) ambapo jumla ya wananchi 721 wamefikiwa na huduma hiyo. Pia kulifanyika zoezi la uchangiaji damu salama, upimaji wa magonjwa yasiyopewa kipaumbele, uchunguzi wa Saratani ya mlango wa kizazi na huduma ya uzazi wa mpango.




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa