• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Mawaziri 8 Wafika Geita, Waahidi Kufikisha Maombi ya Ardhi ya Wananchi kwa Mhe. Rais, Waacha Tumaini”.

Posted on: February 19th, 2019

Jumla ya viongozi wa wizara nane (8) wamewasili Mkoani Geita kwa lengo la kuangalia na kutatua changamoto za ardhi ikiwemo migogoro mbalimbali, ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt, John Pombe Magufuli kusitisha mara moja zoezi la kuviondoa Vijiji na Vitongoji vinavyodaiwa kuwepo katika maeneo ya hifadhi na kuzitaka Wizara zote zinazohusika kukutana ili kubainisha na kuanza mchakato wa kurasmisha maeneo ya Vijiji na Vitongoji hivyo.

Baada ya kupata taarifa ya utangulizi iliyoonesha uhitaji wa jumla ya Hekta za eneo elfu thelathini na mbili (32,000) pamoja na kilometa thelathini (km30) kutoka eneo la mpaka wa hifadhi kuingia ndani ya hifadhi, kiongozi wa msafara huo wa wahe. Mawaziri, Mhe. William Lukuvi (Mb) ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliongozana na Mwenyeji Mkuu wa Mkoa wa Geita kuongea na wananchi wa Bwanga,Wilayani Chato kuwaeleza lengo la ziara hiyo, waliokusanyika kwa wingi baada ya ugeni huo kuwasili katika Uwanja wa Shule ya Sekondari Magufuli tarehe 18.02.2019.

Waziri Lukuvi amewaeleza wananchi kuwa, ”geita ni miongoni mwa mikoa iliyoathirika sana na hifadhi ya misitu kwakua asilimia sabini na tano (75%) ya ardhi ya mkoa huu iko kwenye hifadhi za misitu. Tunatambua mna ardhi kidogo, hivyo kwa maagizo ya Mhe. Rais Magufuli ya kuwapa wananchi ardhi inayowatosheleza kufanya shughuli  za kilimo na ufugaji, tutafikisha maombi yenu yaliyowasilishwa na viongozi wenu ambayo tunaamini yatajibiwa na tunawapongeze kwa kuwa ninyi Chato mliheshimu na vijiji kumi na sita (16) vimepisha msitu, viko nje vimebanana sana”.

Mhe. Lukuvi akachukua fursa hiyo kuwaomba wananchi kuwa wavumilivu wakati wakisubiri majibu ya maombi yao ya ardhi yatakayofikishwa kwa Mhe. Rais Magufuli akiwaomba wasivamie misitu ili kusubiri kupangwa upya watakaporejea tena ili kila kijiji kiwe na eneo lake linalotambulika na wakulima na wafugaji waweze kufanya shughuli zao bila shida yoyote, huku akiwataka viongozi kusimamia wakati huu wa mpito kisha viongozi hao wakaendelea na safari.

Awali, mwenyeji wa ugeni huo Mhe. Mhandisi Robert Gabriel aliwaongoza wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama kuupokea ugeni na kisha kufanya kikao kidogo ukumbini na kutoa taarif fupi kabla ya viongozi hao kuwasalimia wananchi.

Nao Wakuu wa Wilaya za Chato na Bukombe mahali penye changamoto hizo za ardhi wakapata fursa ya kueleza maeneo wananchi wanayohitaji kupewa, ambapo Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mhe. Eng. Mtemi Msafiri aliainisha uhitaji wa eneo la ukubwa wa Hekta 19,000 kutokana na uwepo wa vijiji 16 pembezoni mwa hifadhi ya msitu wa Biharamuro- Kahama na Kwa upande wa Bukombe, Mkuu wa Wilaya Mhe. Said Nkumba akaainisha uhitaji wa eneo la Hekta 13,000 pamoja na km.30 kutoka mpaka wa hifadhi hiyo kuingia ndani.

Ugeni huo Mkoani Geita ulijumuisha Waheshimiwa Mawaziri nane (8), yaani Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Waziri Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Naibu Waziri Kilimo, Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira na Waziri Maliasili na Utalii.  





Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa