• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MDH Watambulishwa Rasmi Geita, Waja na Afya Kwanza

Posted on: February 7th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amefungua kikao cha uhabarishaji na kutambulisha Mradi wa Afya Kwanza unaoratibiwa na Shirika lisilo la Kiserikali la Management Development for Health (MDH), kikao kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa tarehe 06.02.2019.

Akifungua kikao hicho, Mhandisi Gabriel ameanza kwa kuwashukuru na kuwakaribisha MDH ambao wamekuja kwa lengo la kuutambulisha mradi wa Afya Kwanza na kwamba mkoa utaendelea kutoa ushirikiano huku akisisitiza juu ya viongozi kutambua kuwa wana mustakabali wa afya ya wanaGeita, hivyo kutoa maoni yao wakati wa majadiliano kutaleta matokeo chanya.

Amesema, “Kipekee, naomba kutumia nafasi hii kuwashukuru Shirika la MDH kupitia PEPFAR, Shirika la ICAP, Shirika la Intrahealth na wadau wengine wa Mkoa kwa michango yenu ya rasilimali fedha na utaalamu katika kuboresha huduma hapa nchini. Nawakaribisha sana, lakini pia nishukuru kwa jitihada na mikakati mliyonayo ya kuhakikisha jamii ya mkoa wetu inakuwa na afya njema, zaidi katika mkakati wa kupambana na maambukizi ya virusi vya UKIMWI ambapo tunatakiwa kuendelea kufanya vizuri kwenye 90, 90, 90 pamoja na taarifa nzuri niliyoipata kuwa zaidi ya asilimia 90% ya vijidudu vimefubazwa” kisha kufungua kikao na kuomba viongozi kutambua yakwamba wana dhamana kubwa ya kuhakikisha afya ya wananchi inakuwa imara.

Akiutambulisha Mradi wa Afya Kwanza, Meneja Mkuu wa Shirika la MDH Tanzania Bw.Emilian Busara amesema kuwa watakuwa Geita kwa miaka mitano na kwa utaratibu wa kusaini mkataba kila mwaka.  Ameendelea kusema kuwa, shirika hilo linayo malengo yake ikiwemo ya kuhakikisha 90, 90, 90 zinafikiwa yani upimaji, kuanzisha tiba kwa waliobainika kuishi na VVU, uimarishaji wa utoaji wa huduma bora za tiba na matunzo (CTC) kwenye vituo vya afya, vilevile kuimarisha mifumo ya utoaji takwimu za afya.




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa