• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mfumo wa m-mama Kuendelea kwa Ufanisi Mkoani Geita

Posted on: August 21st, 2024


Serikali katika Mkoa wa Geita imeeleza kuwa Mfumo wa Usafirishaji wa Dharura kwa akina mama wajawazito, waliojifungua ndani ya siku 42 na watoto wachanga wenye umri hadi siku 28 (m-mama) utaendelea kutoa huduma na kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa ili lengo la kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi liweze kufikiwa.

Kauli hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Geita Ndg. Herman Matemu alipokuwa mgeni rasmi wakati wa kikao cha makabidhiano ya mfumo wa m-mama kutoka kwa wadau pamoja na kujadili mpango kazi wa uendelevu wake kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita hivi karibuni.


Ndg. Herman Matemu ametoa shukrani za dhati kwa Serikali ya awamu ya sita na wadau wote wa maendeleo ambao ni Vodacom, Touch Foundation na Pathfinder International kwa kuimarisha mfumo wa m-mama  na kuwezesha jumla ya kina mama 3511 na watoto wachanga 538 kusafirishwa tangu ulipoanza utekelezaji katika mkoa wa Geita mwezi Juni 2023.

Mwakilishi wa Katibu Tawala Mkoa wa Geita amesema kuwa ili mfumo huu uendelee kusimama imara na kufanya kazi Halmashauri zote za Mkoa wa Geita zinatakiwa kuhakikisha Bajeti za usafiri wa dharura kwa akina mama wajawazito na watoto wachanga pamoja na gharama za ufuatiliaji zinajumuishwa katika bajeti kuu za Halmashauri kwa kila mwaka.

Mwakilishi wa Shirika la Pathfinder International Bw. Uriel Kinuma ametoa shukrani kwa namna Serikali ilivyoshirikiana nao kama wadau katika kuhakikisha wanapunguza vifo vya wajawazito, waliojifungua na watoto wachanga kwa kuimarisha mfumo wa rufaa na usafiri wa dharura kwa gharama nafuu na kwa kutumia teknolojia tangu ulipoanza kazi katika Mkoa wa Geita na ana matumaini kuwa wadau wanapoukabidhi rasmi kwa Serikali utaendelea kufanya kazi kwa ufanisi mkubwa.

Kwa upande wa mratibu wa m-mama Mkoa wa Geita Bi. Jasintha Boniphace amesema tangu mfumo ulipoanza kazi katika mkoa huo wamefanikiwa kutoa elimu kuanzia ngazi za vijiji hadi Mkoa ikijumuisha Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali kubwa, Kupata madereva ngazi ya jamii ambao wameshaingia mikataba na wakurugenzi wa Halmashauri  pamoja na kuwasafirisha wagonjwa Zaidi ya 4049.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa