• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Minara 55 Yawanufaisha Zaidi ya Wananchi Laki Sita Geita

Posted on: July 23rd, 2024


Zaidi ya wananchi laki sita waishio katika maeneo ya vijijini ndani ya Mkoa wa Geita wamenufaika na ujenzi wa minara 55 ya mawasiliano iliyojengwa na inayoendelea kujengwa katika Wilaya za Nyang’hwale, Geita, Bukombe, Mbogwe na Chato Mkoani humo.

Akizungumza hivi karibuni wakati wa ziara ya ukaguzi wa minara hiyo, Mkurugenzi wa Mfuko wa Mawasiliano kwa wote (UCSAF) Bi. Justina Mashiba ameeleza kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa ruzuku ya shilingi Bilioni 6.44 kwa ajili ya ujenzi wa minara ya mawasiliano kwa teknolojia ya 2G, 3G na 4G ambapo mpaka sasa watanzania 643,354 katika Mkoa wa Geita wamenufaika.

Bi. Mashiba ameongeza kuwa kupitia mfuko wa UCSAF Serikali imeingia makubaliano na watoa huduma za mawasiliano kujenga minara 2,185 Nchi nzima ambapo Zaidi ya wananchi milioni 23 wanaoishi katika vijiji 5,111 watanufaika na mradi huu mara utakapokamilika.

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuupatia Mkoa wa Geita fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa minara ya mawasiliano ambayo itaboresha hali ya mawasiliano kwa wananchi wanaoishi katika maeneo ya vijijini.

Mhe. Shigela ameeleza baadhi ya faida zitakazopatikana kupitia uboreshwaji wa mawasiliano vijijini ni pamoja na kufungua fursa za biashara kwa wananchi waishio katika maeneo hayo ambao wanafanya shughuli mbalimbali za kiuchumi kama kilimo, ufugaji, uvuvi ambao baada ya kupata mawasiliano yenye uhakika wataweza kujitangaza kibiashara kupitia simu janja za mkononi na kupata wateja pasipo kutumia nguvu kubwa.

“Ndugu wananchi wenzangu wa mkoa wa Geita ambao mmeshapata minara katika maeneo yenu, ninawasihi kuitunza vizuri ili baadhi ya vijana wetu wapate ajira ndogo ndogo kupitia minara hiyo pia wakulima, wavuvi, wafugaji na wananchi wengine mtapata fursa ya kuongeza uchumi na kujipatia maendeleo binafsi na jamii nzima kupitia simu zenu za mkononi.” Aliongeza Mhe. Shigela.

Mfuko wa Mawasiliano kwa wote ulianzishwa kwa lengo la kufikisha huduma za mawasiliano vijijini na mjini kusiko na mvuto wa kibiashara. Mkoa wa Geita ni moja kati ya mikoa ambayo ni mnufaika wa mradi ambapo ujenzi wa minara 55 unaendelea katika Wilaya ya Bukombe minara 10, Chato minara 9, Halmashauri ya Wilaya ya Geita minara 10, Mbogwe minara 18 na Nyang’hwale minara 8. Mpaka kufikia mwezi Julai 2024 Minara sita kati ya 55 inayojengwa imeshawashwa.




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa