• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

Posted on: May 27th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mheshimiwa Martine Shigela ametoa pongezi za dhati kwa wasimamizi wa Miradi ya TASAF kwa kuuwezesha Mkoa wa Geita  kuwa Mkoa wa kwanza Kanda ya ziwa kwa utekelezaji mzuri wa miradi ya miundombinu inayotekelezwa kwa fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jamii Nchini (TASAF).

Mhe. Shigela ametoa pongezi hizo hivi karibuni alipokuwa akizungumza katika kikao cha tathmini ya utekelezaji wa miradi ya TASAF ndani ya kipindi cha miaka 5, Kikao ambacho kimefanyika katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita.

Akifungua kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Geita  amewataka waratibu na wakurugenzi kuhakikisha miradi inakamilika kabla ya mwisho wa mwaka wa fedha Juni 30 sambamba na kusisitiza umuhimu wa manunuzi kwenda sambamba na malipo ya mafundi ili kazi zilizopangwa ziweze kukamilika kwa wakati.

Akisoma taarifa ya mapokezi ya fedha za TASAF, Katibu Tawala wa Mkoa Geita Ndg. Mohamed Gombati ameeleza kuwa Mkoa wa Geita katika kipindi cha miaka 5 umepokea Zaidi ya shilingi Bilioni 58 kutoka TASAF, ambapo kati ya fedha hizo shilingi Bilioni 5.3 ni kwa ajili ya walengwa 37,688 kupitia mpango wa uhawilishaji fedha na shilingi 18 Bilioni zimetumika kutekeleza miradi ya maendeleo ya kijamii.

Katibu Tawala Mkoa Geita ameongeza kuwa Mkoa umeongezewa Shilingi Bilioni 18 baada ya kufanya vizuri kwenye utekelezaji wa miradi katika Wilaya za Chato na Mbogwe kwa ajili ya miradi ya afya na elimu ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali za kupunguza umaskini.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Hashim Komba amesema kuwa TASAF imechangia kupunguza utoro katika shule ya Sekondari Izumacheli baada ya kujengewa mabweni ya wanafunzi waliokuwa wakitumia mitumbwi kuvuka maji kila siku kwenda shule na kurudi nyumbani. Pia ametoa ushauri kwa Halmashauri kutenga kwenye bajeti fedha za asilimia 10 ambayo huwa inaongezwa na jamii wakati wa utekelezaji wa miradi ya Tasaf.

Mpango wa TASAF kwa Mkoa wa Geita umewezesha wanafunzi Zaidi ya 89,000 kupata mahitaji ya shule na watoto 7,582 walio na umri chini ya miaka mitano kuhudhuria kliniki kwa ajili ya huduma na elimu ya malezi.





Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa