• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkoa wa Geita Waagizwa Kusimamia Mabaraza ya Ardhi

Posted on: August 30th, 2017


Mkoa wa Geita Waagizwa Kusimamia Mabaraza ya Ardhi

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi  Mh. Angelina L. Mabula ameuagiza uongozi wa Mkoa wa Geita kuhakikisha Mabaraza ya Ardhi yanayoundwa katika Halmashauri zilizoko katika Mkoa yanasimamiwa vyema ili kutekeleza majukumu yaliyokusudiwa.

Agizo hilo limetolewa wakati wa kikao cha majumuisho ya ziara yake kilichowajumuisha viongozi wa Mkoa wa Geita pamoja na Wataalam wa Idara ya Ardhi  katika Ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita tarehe 29/8/2017.

Mh. Angelina Mabula amesema kuwa Halmashauri za Mkoa wa Geita zinatakiwa kuwapa mafunzo ya kuwajengea uwezo wajumbe wa mabaraza ya ardhi wanaochaguliwa ili watambue wajibu wao ikizingatiwa kuwa wajumbe hao hujumuisha watu mbalimbali ambao hawana elimu ya ardhi, hivyo mafunzo hayo yatawapa uelewa wa majukumu yao.

Katika kuhakikisha suala hilo linafanikiwa, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi amesema kuwa Wizara yake iko tayari kushirikiana na Halmashauri kutoa mafunzo ya namna ya kuwapa elimu ya awali wajumbe wa Mabaraza ya ardhi ya Kata na Vijiji. Hivyo Halmashauri zisisite kuwasiliana na Wizara ya Ardhi pindi watakapohitaji huduma hiyo.

Mh. Angelina Mabula ametoa pongezi kwa Halmashauri zote za Mkoa wa Geita kwa utayari wa kushirikiana na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC). Ambapo Halmashauri zote zimeshatenga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za bei nafuu. Pia ameziagiza Halmashauri zote za Mkoa wa Geita pamoja na Shirika la nyumba la Taifa kufanya ufuatiliaji wa vikundi vilivyopatiwa mafunzo ya kufyatua matofali ili kubaini mashine za vikundi ambavyo havifanyi kazi zichukuliwe na kupelekwa katika vikundi vinavyofanya kazi.

Katika ziara yake ndani ya Mkoa wa Geita Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi alitumia fursa hiyo kuwaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri zote na Wataalam wa Idara ya Ardhi katika Mkoa wa Geita kuhakikisha Mfumo wa Usimamizi na Ukusanyaji  kodi za Ardhi kielektroniki unatumika kikamilifu ili kuwezesha ukusanyaji wa mapato unaokidhi malengo yaliyopangwa.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa