• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Mkoa akabidhi milioni 173.5 kwa Vikundi 26 vya Vijana na Wanawake

Posted on: May 22nd, 2018

Mkuu wa Mkoa Geita akabidhi milioni 173.5 kwa Vikundi 26 vya Vijana na Wanawake

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel, amekabidhi mkopo wenye thamani ya shilingi Milioni Mia Moja Sabini na Tatu na Laki Tano  (Tshs.173,500,000) kwavikundi ishirini na sita (26) vyenye jumla ya wanachama Mia Tano Themanini na Tisa (589) ikiwa utekelezaji wa utoaji wa fedha asilimia kumi (10%) ya makusanyo ya ndani leo tarehe 22/05/2018 katika ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita.

Akiwasilisha taarifa kwa mgeni rasmi, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya Wilaya ya Geita, Bw. Ali A. Kidwaka alieleza kuwa, hadi sasa kwenye mpango na bajeti ya Halmashauri kwa mwaka wa fedha 2017/2018, jumla ya Milioni Mia Mbili Ishirini (Tshs. 220,000,000/=) zimetolewa ikiwa ni asilimia kumi (10%) ya mapato ya ndani. Ambapo awamu ya kwanza, hadi kufikia tarehe 30, Aprili mwaka huu, Halmashauri imeweza kutoa jumla ya Tshs. 57,000,000 kwa vikundi 16 vya wanawake na vikundi 10 vya vijana.

Kwa upande wake mgeni rasmi Mhe. Mhandisi Gabriel alianza kwa kuwashukuru wanavikundi kwa mahudhurio yao mazuri na kuzidi kusisitiza Azma na Sera ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuelekea Tanzania ya viwanda, kwa lengo la kumkomboa mwananchi maskini ili aweze kujishughulisha na kujiajiri yeye mwenyewe na kuwa na maisha bora. Alikemea migogoro ndani ya vikundi inayosababisha vikundi vingi kusambaratika baada ya kupewa mikopo hivyo kupelekea ucheleweshwaji wa mikopo kupitia msemo katika msafala wa Mamba, Kenge pia wamo.

Alimaliza kwa kusema “serikali kwa kupitia wataalam wake, haitaweza kufumbia macho vikundi vya aina hii na sheria kali itachukuliwa dhidi ya vikundi hivyo”. Lakini pia aliwakumbusha wanavikundi kwa msemo wa kijasiliamali usemao “mali bila daftari, hupotea bila habari” na kuwaomba wadau wa maendeleo na taasisi za kifedha kuendelea kutoa elimu ya utunzaji fedha, kisha kukabidhi mikopo hiyo.

Pongezi kwa ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji kupitia, Idara ya Maendeleo ya Jamii, Timu ya Ukusanyaji wa Mapato, Kamati ya Mikopo, Wanasheria na Waheshimiwa Madiwani wote kwa pamoja katika kuhakikisha mapato yanakusanywa na asilimia 10 ya makusanyo inawafikia walengwa.  

Miongoni mwa waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mwenyekiti na Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya, Wawakilishi wa NSSF, CCM, NHIF, NMB, TRA, LAPF na SIDO


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa