• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MKUU WA MKOA ATOA ONYO KWA VIONGOZI WANAOTUMIA MICHANGO YA WANANCHI KWA MASLAHI BINAFSI BUKOMBE

Posted on: November 14th, 2017

MKUU WA MKOA ATOA ONYO KWA VIONGOZI WANAOTUMIA MICHANGO YA WANANCHI KWA MASLAHI BINAFSI BUKOMBE

Viongozi wa vijiji, kata na tarafa Wilayani Bukombe wametakiwa kutumia michango inayotolewa na wananchi kwa shughuli zilizokusudiwa ili kuwaletea wananchi maendeleo katika maeneo yao.

Akizungumza katika kijiji cha Kazibizyo kata ya Ng'anzo Wilaya ya Bukombe Mhandisi Robert Gabriel Mkuu wa Mkoa wa Geita amesema katika  vijiji, kata na tarafa wananchi wamekuwa wakihimizwa kujitolea kuchanga michango ya hiari ili kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo lakini baada ya michango hiyo kukusanywa inatumika kwa maslahi binafsi ya Viongozi.

Amesema kuwa Viongozi hao wasio na maadili  wanapanga matumzi ya fedha za wananchi bila kujali vipaumbele vya vijiji kwa maslahi yao binafsi vitendo hivyo vinawavunja moyo wananchi wa kutoendelea kutoa michango ya maendeleo. "Kuna vidudu vinavyoleta magonjwa watu wanasubili maendeleo hayatokei inabidi tuvitoe tuvipige sindano kubwa vife humu humu viongozi wa namna hiyo wasio na maadili wamekuwa wakihamishwa wakati hawajatoa taarifa za mapato na matumizi alah! kama yupo Geita arudi arejeshe fedha za wananchi popote alipo". 

Amesema kama kuna mtu au mtendaji anayeona hatoshi apishe akae pembeni ili wanaoweza kufanya kazi wafanye ili kuleta maendeleo ya haraka kwa wananchi. Hata hivyo, ametoa wito kwa wananchi kutumia rasilimali zinazowazunguka kujiletea maendeleo badala ya kukaa na kulalamika maisha magumu wakati kuna rasilimali nyingi katika maeneo wanayoishi.  Aidha, amezitaka Halmashauri Mkoani Geita kusajili na kuvitumia vikundi vya mafundi vinavyojitolea kujenga madarasa na Zahanati bila malipo katika miradi ya fedha katika maeneo mbalimbali ili vijana hao wanufaike badala ya kutoa kazi zote kwa wakandarasi.

Awali  Josephat Maganga Mkuu wa Wilaya ya Bukombe amemweleza Mkuu wa Mkoa kuwa Wilaya ya Bukombe ina vijiji 52 na Vitongoji 372 lakini kuna Zahanati sita (6) tu za Serikali.  Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel akiwa Wilayani humo amezindua kampeni ya ujenzi wa vyumba vya madarasa na Zahanati katika vijiji vya Kazibizyo na Bulama kwa kushiriki katika ujenzi na harambee iliyoleta michango ya mifuko 93 ya simenti, fedha tasilimu  shilingi 340000/=, tofali 500,mbao 50 na misumari kilo3.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa