• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MPANGO KABAMBE WA MAENDELEO YA MJI KUINUA UCHUMI WA MKOA-GEITA

Posted on: November 21st, 2017

MPANGO KABAMBE WA MAENDELEO YA MJI GEITA KUINUA UCHUMI WA MKOA

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel amewataka wadau wa maendeleo ya Mkoa wa Geita kutumia fursa zinazopatikana katika mkoa huo na namna ya kuzitumia ili kuboresha maisha ya wananchi na kuinua uchumi kwa ujumla.

Akizungumza katika ufunguzi wa kikao cha kujadili mpango kabambe wa maendeleo ya Halmashauri ya Mji wa Geita 2017-2037 hivi karibuni katika ukumbi wa Halmashauri ya Mji, Mhandisi Robert Gabriel amesema kuwa fursa kama uwepo wa eneo la kanda ya madini, mazi wa makuu, misitu ya asili, bonde lenye rutuba kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji na barabara zinazounganisha mji huo na maeneo ya jirani zipangiwe mikakati itakayo wakwamua wananchi kiuchumi. “Mzingatie kuwa Halmashauri  ya Mji Geita ndipo makao makuu ya Mkoa wa Geita na kitovu cha utawala na ukuaji wa uchumi wa mkoa ambapo shughuli zote za kiutawala, kijamii na kiuchumi zinafanyika, Hivyo Mpango kabambe ni muhimu kutekelezwa.” Aliongeza Mhandisi Robert Gabriel.

Mhandisi  Robert Gabriel amesema kuwa mji wa Geita unatoa soko la mazao kwa shughuli zinazofanyika katika wilaya hii, shughuli za usafirishaji, utalii, utawala, afya, elimu na benki hivyo ni vema uhusiano uliopo ukajadiliwa kwa kina ili kuleta chachu ya maendeleo kwa miji na maeneo yote yanayozunguka mkoa kwa ujumla.

Akieleza umuhimu wa mpango huo Mkuu wa Mkoa wa Geita amefafanua kuwa endapo mpango huo utatekelezwa vizuri utapunguza kero za viwanda vinavyotoa hewa chafu ambavyo viko pamoja na makazi ya watu, sehemu za kuabudia pamoja na maeneo ya starehe na baa zilizojengwa katikati ya makazi ya watu.

Afisa Mipango Miji wa Halmashauri ya Mji Geita Ndg. Oswald Cassian amesema kuwa mpango kabambe ni dira ya kuongoza, kusimamia na kudhibiti maendeleo ya ardhi kwenye sekta zote zinazotumia ardhi kama vile afya, elimu, barabara, maji, umeme, makazi/ viwanda na mengineyo. Mpango huo ulianza kuandaliwa na Halmashauri kwa kushirikiana na wataalam kutoka Wizara ya Ardhi, nyumba na maendeleo ya makazi mwaka 2014.

Mji wa Geita ni moja kati ya miji 18 inayofadhiliwa na mradi wa ULGSP chini ya ufadhili wa Benki ya Dunia, ambapo mpango kabambe ni moja ya mradi unaofanyika chini ya mpango huo. Kauli mbiu ya mpango huoni “MPANGO KABAMBE WA MJI WA GEITA KATIKA KUSIMAMIA UENDELEZAJI WA RASLIMALI ZA MADINI YA DHAHABU”.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa