• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MWENGE WA UHURU WABORESHA HUDUMA ZA AFYA NKOME

Posted on: October 6th, 2024


Zaidi ya Wananchi elfu 43 wa Kata ya Nkome na maeneo ya jirani watanufaika na maboresho ya  huduma za afya zitakazotolewa baada ya upanuzi wa Zahanati ya Kata hiyo kuwa Kituo cha Afya kukamilika mwishoni mwa mwezi Oktoba mwaka 2024.

Akizungumza wakati wa uwekaji jiwe la msingi katika Kituo cha Afya Nkome, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 Ndugu. Godfrey Eliakimu Mnzava amesema kuwa nia ya Serikali ya awamu ya sita ni kuhakikisha Sekta ya Afya inaboreshwa ili wananchi waweze kuhudumiwa katika viwango vinavyokubalika.

Ndg. Godfrey Mnzava ameongeza kuwa ujenzi wa majengo matatu ya Maabara, Wodi ya wazazi na jengo la wagonjwa wa nje kutatoa fursa kwa wagonjwa watakaokwenda kupata huduma kuwa na eneo kubwa lisilowabana, kadhalika na watoa huduma kupata nafasi itakayowatosha kuwahudumia wagonjwa wanaofika kituoni kwa ajili ya huduma.

Mbunge wa Jimbo la Geita vijijini Mhe. Joseph Kasheku Msukuma ametoa shukrani kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mgodi wa Dhahabu Geita kwa kuiwezesha Kata ya Nkome na kuweka kumbukumbu ambayo haitafutika katika vichwa vya wananchi wa Nkome kutokana na ongezeko la majengo katika Kituo cha Afya Nkome.

Mhe. Msukuma ameongeza kuwa  Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 umefanyika chachu kwa viongozi wa Serikali katika Wilaya ya Geita na wananchi [J1] wa Kata ya Nkome kuona umuhimu wa upanuzi wa Zahanati ya Kata kwenda kuwa kituo cha Afya ili kuongeza huduma ambazo awali zilikuwa zikitolewa nje ya Kata hiyo na kuwalazimu  wananchi hususan wanawake, watoto na wazee kufuata huduma hizo mbali pale inapohitajika.

Mwenge wa Uhuru 2024 umehitimisha ziara yake katika Mkoa wa Geita ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita ambapo umekimbia umbali wa kilomita 44.1 na kukagua, kutembelea, kuweka jiwe la msingi na kuzindua miradi 11 yenye gharama ya Shilingi Bilioni 2.8




[J1] e




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa