• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mwenge wa Uhuru Wapongeza Ujenzi wa Ofisi Geita DC

Posted on: September 2nd, 2025


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2025 Ndugu Ismail Ali Ussi ameridhishwa na kutoa pongezi za dhati kwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa ujenzi wa Ofisi bora na ya kisasa kwa ajili ya wataalam wa kada mbalimbali wanaofanya kazi katika Kata ya Bugulula.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru ametoa pongezi hizo alipokuwa akizindua mradi wa Ofisi ya Kata ya Bugulula, Mwenge wa Uhuru ukiwa katika mbio zake ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Geita tarehe 1 Septemba 2025.

Ndg. Ismail Ali Ussi ameeleza kuwa dhamira ya Serikali ya awamu ya sita ni kuhakikisha wataalam wake wanapata mazingira rafiki ya ufanyaji kazi na wananchi wa kata zote Nchini wanapatiwa huduma za utatuzi wa changamoto mbalimbali katika maeneo ya jirani na makazi yao ndio sababu wakurugenzi wa Halmashauri zote wamesisitizwa kutenga fedha za mapato ya ndani kwa ajili ya ujenzi wa Ofisi za vijiji, mitaa na kata.

“Miaka ya nyuma ilikuwa ni ndoto kuona ofisi ya Serikali tena katika ngazi ya kata imejengwa kisasa na katika ubora wa hali ya juu utadhani hoteli, lakini Ofisi ya Kata ya Bugulula ambayo iko Geita vijijini imejengwa katika mfanano wa hoteli ya kisasa iliyopo mjini, hili ni jambo la kujivunia uongozi imara wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na pia nitoe pongezi za dhati kwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita kwa kufanikisha ujenzi huu kwa kutumia mapato ya ndani ya Halmashauri.” Aliongeza Ndg. Ismail Ali Ussi.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita, Mtendaji wa Kata ya Bugulula Bw. Juma Gorwe Choma amesema kuwa ujenzi wa ofisi hiyo ulioanza mwezi Februari 2025 umetumia jumla ya shilingi Milioni 144,704,000/= ambapo kati ya fedha hizo shilingi 846,000/= zikiwa ni nguvu za wananchi wa Kata ya Bugulula.

Bw. Juma Choma ameeleza kuwa faida ya Ofisi hiyo ni pamoja na kusogeza huduma karibu na wananchi kwa kuwa huduma zote za kiutawala zitapatikana katika jengo moja, kadhalika mradi huo utatoa suluhisho na kupunguza gharama kwa kulipa kodi katika majengo ya watu binafsi walipokuwa wamepanga awali.

Ukiwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mwenge wa Uhuru umetembelea, kufungua, kuzindua, kuweka mawe ya msingi na kukagua jumla ya miradi tisa yenye thamani ya shilingi za kitanzania Bilioni 2.8 ukiwa umebeba Kauli Mbiu isemayo “JITOKEZE KUSHIRIKI UCHAGUZI MKUU WA MWAKA 2025 KWA AMANI NA UTULIVU”.

Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Mwenge wa Uhuru Wapongeza Ujenzi wa Ofisi Geita DC

    September 02, 2025
  • Zaidi ya Vijana Zaidi ya 12,000 Kujikwamua Kiuchumi Kupitia EACOP

    August 19, 2025
  • GESECO Kinara Mtihani wa Mock Kidato cha NNne Kanda ya Ziwa

    August 19, 2025
  • Serikali Yatoa Zaidi ya Bilioni 40 Kujenga Miundombinu ya Umwagiliaji Geita& Mwanza

    August 12, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa