• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Ndugu viongozi tusiwaze Ushuru tu wa Mazao, naomba tuwasaidie Wakulima” Mhe. Bashe.

Posted on: August 4th, 2020

Mhe. Hussein Bashe Naibu waziri wa Kilimo ameziagiza Taasisi zilizo chini ya Wizara yake zinazoshughulika na huduma za kimaabara kupunguza gharama za huduma hizo ili kuhakikisha Upimaji wa afya ya udongo kwa Wakulima inakua ni huduma na sio biashara kwani itawasaidia wananchi kutambua afya ya udongo kwa mazoa wanayolima na kujua watumie mbolea ya aina gani.

Mhe. Bashe ameyasema hayo jana Jumatatu, Agosti 08, 2020 wakati akifungua Rasmi maonesho ya Kilimo na Sherehe za nane nane kwenye Viwanja vya Nyamhongolo jijini Mwanza ambapo Mikoa ya Mwanza, Geita na Kagera wananakutana hapo kwa juma zima kukamilishamaonesho kwa Kanda ya Ziwa Magharibi.

Aidha, Mhe. Bashe amewasihi viongozi wa Mikoa na wilaya nchini kuhakikisha wanawalea Wakulima kwa kuwatafutia Masoko ya bidhaa na Mazao yao ili kuwaongezea kipato kwa mmoja mmoja na kukuza Uchumi.

Akitoa salamu, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Robert Gabriel amewasihi wananchi waliofika kwenye maonesho hayo na wataoendelea kufika kujifunza kwa kina yatolewayo ili nao wakawaambie Wakulima majumbani wataporudi kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kupeleka ujumbe kwa haraka zaidi kwa wananchi.

Vile ile Mkuu wa Mkoa wa Geita ametambulisha maonesho ya Teknolojia ya madini yanayotarajia kufanyika Kitaifa Mkoani Geita ifikapo mwezi watisa mwaka huu kuanzia tarehe 17 hadi 27. Amewasihi wananchi Kuhudhuria kwa wingi bila kukosa kwani ni fursa ya kujifunza Teknolojia ya madini ambapo maonesho hayo yanafanyika kwa mwaka wa tatu mfululizo.

Wakati huo huo, Mhe. Mkuu wa Mkoa ametembelea mabanda mbalimbali ya maonesho kwenye iwanja hivyo ambapo amefurahisha na uthubutu wa makundi mbalimbali waliojitokeza kuonesha bidhaa zao na ipando ya Mazao mbalimbali viwanjani apo.

Aidha, mku wa Mkoa amefika kwenye banda la Halmashauri nya wilaya ya Bukombe ambapo amekutana na kikundi cha Bora Kilimo Biashara wanaojishughulisha na uchakataji wa Mazao ya Nafaka mabapo amewapongeza kwa kazi nzuri ya ujasiriamali nao kwa kupitia msemaji wao bwana Wilson Mola walimwonesha furaha yao kwa kuishukuru Halmashauri ya wilaya ya Bukombe kwa kuwakopesha Fedha Milioni 36 ambazo zimesaidia sana kukuza biashara yao.

Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Geita amepata fursa ya kuonana na vikundi mbalimbali walio na bidhaa bora zsana kwenye mabanda ya Halmashauri za Chato, Mbogwe na Geita na Mji wa Geita ambapo pamoja na kunywa Mvinyo utokanao na Matunda ya Mananasi vilevile alipata fursa ya kunywa juice nzuri inayotengenezwa kwa kutumia viazi lishe.

Maonesho ya Kilimo na Sherehe za nane nane mwaka 2020 yenye Kauli  mbiu; Kwa maendeleo ya Kilimo, Mifugo na uvui, chagua viongozi bora 2020 yamefanyika Kitaifa kwenye kanda ya Ziwa Mashariki huko Mkoani Simiyu kwenye viwanja vya Nyakabindi ambapo yamefunguliwa Rasmi Agosti 01, 2020 na Mhe. Samia Suluhu, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo yatahitimishwa ifikapo Agosti 08, 2020.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa