• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Ni Vigumu kwa Taasisi Kupata Matokeo Chanya Kama Hakuna “TAPE”, Asema RAS Geita

Posted on: June 21st, 2019

Katika mwendelezo wa Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma, Katibu Tawala Mkoa wa Geita Bw. Denis Bandisa ameendelea kutekeleza programu iliyoandaliwa na mkoa huu ya namna ya kuadhimisha wiki hii, kwa kukutana na kufanya kikao na watumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita na Geita Mji katika Ukumbi wa Mikutano wa GEDECO uliyopo Halmashauri ya Mji Geita juni 21, 2019

Akizungumza kwa nyakati tofauti, Bw. Bandisa amewaasa watumishi wa umma, juu ya kuwa na nidhamu kazini, kuwa wawazi na wawajibikaji wakitambua kuwa, hakuna haki bila wajibu wanapotekeleza majukumu yao lakini pia ushirikiano baina yao ndiyo utakaoleta matokeo chanya huku akiwapa kanuni ya “TAPE” kama kifaa muhimu kitakachoivusha taasisi.

Amesema, “watumishi wa umma, ni vyema mtambue majukumu yenu kwa mujibu wa mkataba, muwe na mpango kazi wa utekelezaji wa shughuli zenu za kila siku. Wenye kasoro mjirekebishe, tujenge mahusiano mema kazini, lakini vile vile tuwe mabalozi wa kuelimisha wananchi juu ya uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliyopo mbele yetu ili waitumie haki hiyo kikamilifu. Ningependa mtumie kanuni ya TAPE katika kufanya kazi zenu, mtafanikiwa”.  

Bw. Bandisa ametoa tafsiri ya neno TAPE akimaanisha T-Transparency yaani (Uwazi), A-Accountability yaani (Uwajibikaji), P-Participation yaani (Ushirikishwaji) na E-Equity yaani (Usawa), ikiwa na maana kuwa, wakuu wa idara na vitengo wana wajibu wa kushirikiana na watumishi wengine kufanya kazi uwazi, ushirikishwaji, usawa na uwajibikaji na kuwasihi kukusanya mapato pamoja na kuwa na miradi ya kimkakati ya kiuchumi.

Awali katika kikao hicho, Meneja wa Mkoa wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) Bw. Odhiambo Elius, aliweza kuongea na watumishi hao akikusanya maoni na changamoto zinazowakabili huku akitoa fafanuzi za masuala mbalimbali yaliyoulizwa na kuwasihi watumishi kuwashawishi ndugu, jamaa na marafiki ambao ni wakulima kujiunga na Mpango Maalum wa Bima ya Afya kwa Wakulima Walio Katika Vyama vya Ushirika wa Mazao (AMCOS) ujulikanao kama “Ushirika Afya” , mpango utakaowawezesha kupata huduma za afya.

Kikao hicho kimehudhuriwa na wakuu wa idara mbalimbali na vitengo kutoka ofisi ya mkuu wa mkoa wa geita, wawakilishi wa wakurugenzi wa halmashauri hizo bila kusahau watumishi wa ngazi zote wa halmashauri zote mbili.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa