• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Nipo Geita Kuhakikisha Tunasonga, Tunapata Maendeleo, Asema RAS Bandisa

Posted on: November 2nd, 2018

Katibu Tawala Mkoa wa Geita Bw. Denis I. Bandisa amesema yupo Mkoani Geita kwa lengo la kufanikisha shughuli zote za maendeleo bila kupendelea upande wowote.
Amesema kauli hiyo tarehe 01.11.2018 wakati wa kikao maalum cha Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Geita kufuatia Madiwani hao kutokuwa na uelewa juu ya maelekezo yaliyokuwa yametolewa kwenye kikao cha baraza hilo awali tarehe 27.10.2018 juu ya upandishwaji hadhi kituo cha Afya Nzera kuwa Hospitali ya Wilaya kilichopo Jimbo la Geita, jambo lililopelekea fedha kiasi cha Shilingi Bilioni Moja, Milioni Mia Tano kuelekezwa sasa kwenye Hospitali ya Wilaya Nzera.

Akitoa ufafanuzi wa suala hilo Bw.Bandisa alianza kwa kusema, “wahe. Madiwani, tambueni ya kuwa, nimeteuliwa kuja kuisaidia Geita isonge mbele kimaendeleo bila upendeleo wa mahali popote, hivyo niwaombe mpendane, mshikamane, muwe kitu kimoja kwenye suala zima la maendeleo lakini pia kama kuna jambo mnahitaji ushauri basi msisite kufika ofisini niko tayari kuwasaidia”.

Bw. Bandisa amewaelekeza Madiwani hao kuwa, wanapaswa kutambua kwamba  Serikali inaendeshwa kwa mujibu wa Sheria, Taratibu na Kanuni hivyo basi kama kuna jambo halijaeleweka ama kukubaliwa ni vyema kufuata njia sahihi kutatua changamoto ili kwenda pamoja kwakuwa nia ni kujenga akiwahakikishia kuwa Kituo cha Afya Katoro kitaendelea kuboreshwa lakini pia kampeni ya ujenzi wa zahanati kila kijiji, kituo cha Afya kila kata vitakua ni suluhu ya muda mrefu na vitapunguza msongamano kwenye Hospitali za Rufaa. Pia amewashauri wajumbe wa Baraza hilo kujenga hoja kwa kutumia fursa na changamoto wanazokumbana nazo na si kupingana na maagizo na maelekezo ya Serikali yanapokuwa yametolewa.


Mbunge wa Jimbo la Busanda Mhe. Lolesia Bukwimba, awali hakuwa amekubaliana na fedha hizo kupelekwa Hospitali ya Nzera lakini baada ya ufafanuzi uliyotolewa na Katibu Tawala ilionekana ni vyema kuwa na mbadala kutokana na ukweli kuwa bado kuna uhitaji wa kuwa na Hospitali yenye hadhi ya Wilaya Mamlaka ya Mji Mdogo wa Katoro kulingana na idadi ya watu waliyopo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Mhe. Elisha Lupuga amewashukuru wajumbe hao kwa ukubali wao juu ya maagizo ya Serikali huku akisisitiza kuwa wamoja, wenye kuheshimiana na kupendana wakitambua kuwa jambo linapofanyika jimbo mojawapo basi ni kwa nia ile ile ya kuleta maendeleo na si vinginevyo. Amewashauri pia kutumia uzoefu wa Katibu Tawala Mkoa ili kufanikisha mipango yao kwakuwa anaamini kuwa mtumishi huyo ameletwa Geita si kwa bahati mbaya bali ni msaada muhimu sana wamtumie. Kisha Mwenyekiti Lupuga akawasamehe wajumbe ambao awali alitaka kuwapeleka kwenye kamati ya maadili vilevile akawataka Madiwani wote kwenda kufanya mikutano na Kamati za Maendeleo za Kata (WDC) ili kuona ni miradi gani itatekelezwa na fedha za Miradi ya Jamii (CSR).

Naye Mkuu wa Wilaya ya Geita Mhe. Josephat Maganga amewaeleza wajumbe wa Baraza hilo kuwa, matatizo yapo pande zote yaani jimbo la Busanda na Geita kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Geita ina majimbo mawili hivyo kuchelewesha maamuzi ni kuchelewesha maendeleo lakini pia kupoteza rasilimali fedha na muda.

Mwisho Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Geita Bw. Ali Kidwaka akawasihi Wahe.Madiwani kutopenda kuwa na migogoro ndani ya Halmashauri kwani inachelewesha maendeleo.





Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa