• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

NMB yafungua Tawi la 229 Mbogwe. RC Gabriel Awaambia “Hamjakosea Kuwekeza Geita” Na Boaz Mazigo, Geita.

Posted on: April 25th, 2019

Katika kuthibitisha kaulimbiu ya Benki ya NMB “Karibu Yako”, Benki hiyo imefanikiwa kufungua tawi la 229 katika Mji wa Masumbwe Wilayani Mbogwe, hafla iliyohudhuriwa na viongozi mbalimbali pamoja na wananchi.

Akiongea wakati wa akifungua Tawi hilo Aprili 25, 2019, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ameelezwa kufurahishwa na uamuzi wa Benki hiyo kuamua kuwekeza katika Wilaya ya Mbogwe Mkoani Geita hususan mji wa kibiashara Masumbwe.

Mhandisi Gabriel amesema,“nawapongeza sana NMB kwa kuchagua kuja Geita, hamjakosea, mmefanya uamuzi sahihi. Pia nipongeze hatua yenu kuthibitisha kauli yenu isemayo “karibu yako” kwakuwa nimeelezwa kuwa awali wateja wenu walitembea umbali wa kilomita 50 kuifikia huduma yenu, hongereni sana”

Hakuishia hapo, Mhandisi Gabriel aliwahimiza wananchi kupenda kuhifadhi fedha zao kwenye Benki kwa usalama zaidi kwakuwa ulimwengu umebadilika. Amewakumbusha wanananchi juu ya matumizi mazuri ya fedha na kuweka akiba akisema “usikope fedha ili kuweka heshima baa”, vilevile kujitahidi kurudisha mikopo wanayowezeshwa ili taasisi iweze kuendelea na kuwahimiza viongozi wa wilaya hiyo kuleta mpango kabambe wa upangaji mji ili kukuza miji kwa kuipanga na kuuza ardhi, kisha akakata utepe na kuweka jiwe la ufunguzi na huduma zikaanza rasmi.

Akitoa taarifa kabla ya mgeni rasmi kuongea, Donatus Richard, Mkuu wa Kitengo cha Biashara NMB, ametaja mafanikio kedekede ikiwemo Benki hiyo kuwa na mashine za kuchukulia fedha (ATM) zaidi ya 800 nchini na mawakala zaidi ya 700. Amesema pia, kwa uwepo wa Soko la Dhahabu Geita wameona ni vyema kusogeza huduma karibu ikiwa ni miongoni mwa njia ya kuthibitisha kuwa NMB ipo bega kwa bega na serikali, huku akiwashukuru wateja kwa kuwa wavumilivu na kuwaomba kutumia vyema huduma zitolewazo na benki hiyo kama vile akaunti ya FANIKIWA kwa ajili ya kuwawezesha wajasiliamali kwa kupatiwa mikopo

Richarch ameendelea kueleza kuwa, Benki ya NMB ni mdau mhamasishaji wa ulipaji kodi mbalimbali za serikali ambapo hadi sasa, tayari jumla ya Wilaya 168 zimeunganishwa na mifumo ya kielekroniki ya ulipaji wa kodi za serikali.

,Mkuu wa Wilaya hiyo Martha Mkupasi, akatumia wasaa huo kuwapongeza NMB kwa kuitikia wito aliokuwa amewaomba kuufanyia kazi kwa muda mrefu kwa kutambua uhitaji wa huduma ya Benki hiyo wilayani hapo, hivyo akawasihi wananchi kukopa na kukuza mitaji yao kibiashara.

Tawi hilo linatajwa kama suluhu ya kupunguza umbali kwa wa km 50 kutoka masumbwe kwenda Bukombe, na Km 50 kutoka Masumbwe kwenda Kahama ambapo awali wateja wa NMB walilazimika kuzifuata huduma hizo kwa umbali huo.

Mojawapo ya sifa ya Benki ya NMB ni ile ya kuonesha tumaini kwa kuweka kibao cha kuonesha umbali wa kilomita chache kuingia mijini karibia kila mahali ilipo, kweli NMB KARIBU YAKO.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa