• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Nyang’hwale Yamthibitishia RC Geita Safari Mpya ya Mabadiliko, Yajipanga kwa Hati Safi

Posted on: July 16th, 2019

Katika kuhakikisha Halmshauri zote za mkoa wa geita zinapata hati safi, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ameendesha mkutano maalum wa baraza la madiwani kujadili hoja za mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2017/2018 (hoja zilizosababisha halmashauri hiyo kupata hati chafu), mkutano uliokuwa na matokeo chanya baada ya wajumbe wa mkutano huo kunuia kupata hati safi kwa miaka baada ya mwaka huo wa fedha walipoketi julai 16, 2019 katika ukumbi wa mikutano, halmashauri ya wilaya ya Nyang’hwale.

Akiongea kabla ya kuweka kikao wazi, mwenyekiti wa mkutano mhandisi Robert Gabriel amewaeleza wajumbe hao kuwa, kikao hicho ni muhimu na cha kipekee kwani kitatoa njia na mwelekeo sahihi wa kuondokana na hati isiyo safi na kisha baada ya majadiliano kuwapongeza wajumbe kwa michango inayoashiria kuwa wamejipanga kupata hati safi akisema kutenda kosa si kosa bali kurudia kosa.

“leo mmedhihirisha sasa tunaanza safari ya mabadiliko, lakini ni muhimu tuwe wawazi kwa fedha yoyote inayoingia ili kuwe na uelewa wa pamoja baina ya wataalam na madiwani. Vilevile mkaguzi wa ndani anatakiwa kutoa taarifa mara moja kupitia taarifa ya robo kila aonapo viashiria vya hoja ili tuidhibiti mapema, hivyo nitoe rai ya upatikanaji wa majibu ya hoja 44 zilizobaki kati ya 66 ndani ya wiki 2 na tujipange kuepuka hati chafu” amesema mhandisi Gabriel.

Taarifa ya mkaguzi wa ndani kuwasilishwa kwa madiwani kila robo pamoja na ukusanyaji wa mapato ili kuiwezesha taasisi hiyo kujiendeshe ikawa ni agizo kwa halmshauri hiyo.

Utunzaji wa nyaraka na uwazi vimekuwa ombi la wajumbe wengi, jambo lililopelekea mhandisi Gabriel kusisitiza watumishi kutunza nyaraka na kuwa wawazi wakishirikiana kisha kumpongeza mbunge wa jimbo hilo Hussein Amar kwa kujitolea kuleta maendeleo nyang’hwale hata kwa fedha zake binafsi.

Mbunge wa Nyang’hwale Hussein Amar kwa upande wake amesema, usiri ndiyo changamoto ya matatizo mengi hivyo ni vyema kuwa wawazi huku akiomba RC Gabriel kumfikishia ombi Mhe.Rais Magufuli kufanya ziara jimboni kwake ikiwa wananchi wanayo shahuku ya kutembelewa na kiongozi huyo

Katibu tawala mkoa Denis Bandisa yeye amewaeleza wajumbe kuwa, ili kutoka hapo walipo, wanahitaji kushirikiana na kusaidian kuanzia menejimenti ya halmashauri pamoja na watumishi bila kusahau madiwani ili kuiondoa kero ya hati isiyosafi.

Mustafa Mwangaile Kwaniaba ya Mkaguzi wa Nje Geita katika taarifa yake amesema, hoja 44 ambazo hazijapata majibu kati ya 66 zimegawanyika katika makundi manne kama vile, kutowasilishwa kwa hati za malipo, kuhamishwa kwa fedha bila kuonekana matumizi, upotevu wa vitabu vya kukusanyia mapato pamoja na malipo yaliyofanyika bila nyaraka kuwasilishwa.

Mkuu wa wilaya hiyo Hamim Gwiyama amewataka watumishi kujitathmini kwa kuhakikisha hawarudii makosa yaliyofanywa na watangulizi katika nafasi walizonazo akisema, hati hiyo isiyosafi imepatikana kutokana kukosa uadilifu, uwazi, utawala bora, uzalendo, ushirikishwaji, uwajibijaki n.k huku akitoa uzoefu wake akisema “uhasibu hauna siasa, nimekuwa mhasibu kwa miaka 20 sikuwahi kupata hati chafu bali safi wakati wote, hivyo jitathiminini kwenye hayo maeneo mtavuka” kisha kuwaasa kufuata maelekezo ambayo yamekuwa yakitolewa na sekretarieti ya mkoa.

Kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri hiyo Mariam Chaurembo amesema, wao wamejipanga na kwa sasa miradi mingi inakwenda kwa kasi ya kuridhisha ikiwemo ujenzi wa hospitali ya wilaya uliyo katika zaidi ya 70% ya utekelezaji, ujenzi wa maboma ya shule ya msingi 9 kwenye kata 10 na maboma mwengine 21 yakiwa na 95% kwa kuzingatia thamani ya fedha huku akishukuru ushirikiano kutoka ofisi ya katibu tawala mkoa wa geita.

Mwenyekiti wa halmashauri hiyo Isack John kwaniaba ya halmashauri akamuahidi RC Gabriel kuyafanyia kazi yote yaliyoelekezwa na kwamba mwaka huu watapata hati iliyo safi.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa