• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Padri Bilingi Atimiza Ahadi, Atua Ofisi ya RC Geita na Miche 1,200 ya Mikwaju

Posted on: December 7th, 2018

Ni jumatano angavu ya terehe 06.12.2018 iliyobarikiwa kwa hali nzuri ya hewa, ndipo Padri Thomas Kabika Bilingi, Chapleini wa Hospitali ya Sengerema anakanyaga malango ya ofisi ya mkuu wa mkoa wa geita.

Baada ya kufika na kupokelewa, ndipo alipoeleza nia ya ujio wake akisema “leo nimekuja kutimiza ahadi yangu kwa Mhe.Mhandisi Robert Gabriel, Mkuu wa Mkoa wa Geita niliyoitoa wakati wa Kumzika marehemu dada wa Mhe. Constantine Kanyasu mwezi Agosti, 2018 katika kijiji cha Nyamboge Halmashauri ya Wilaya ya Geita. Nimeleta miche ya mikwaju elfu moja mia mbili (1,200) itakayogawiwa kwa Halmashauri zote Sita (6) kwa maana ya miche mia mbili (200) kwa kila Halmashauri”.

Ameeleza kuwa, kutoa miche ya miti hiyo kwa kisukuma ikiitwa “mishishi” na Kizinza “misisa”imekuwa ni desturi yake kila anapohudumu kwenye mazishi na kila anapofungisha ndoa huku akihamasisha miche hiyo itunzwe, ikuzwe kwaajili ya dawa, chakula (Sharubati) na utunzanji wa mazingira. Vilevile, Padri huyu anatoa miche hiyo kwakuwa amezaliwa kwenye kijiji kiitwachwo “Kasisa” (mane yake kuna mishishi mingi) kilichopo Halmashauri ya Buchosa ambapo miti hiyo hupatikana kwa wingi.

Amesema, miche hiyo hutoa matunda baada ya miaka nane (8) na ni mizuri haiharibiki hovyo na kwamba bado anayo hazina ya kutosha akisema ataendelea kuipanda miti hiyo hadi umauti utakapomkuta.

Ameeleza kuwa, bado anaendelea kuotesha miti hiyo na anayo mingi na kwamba baada ya kuona miti hiyo inafyekwa sana na watu akaona ni vyema aingie kwenye shughuli ya utunzaji mazingira, ni tangu aadhimishe miaka arobaini (40) ya Upadre na miaka hamsini na tano (55) ya Ubatizo wake katika miaka sitini (60) ya parokia mwaka 2017.

Akipokea miche ya miti hiyo kwa niaba ya Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Bw.Deodatus Kayango ambaye pia ni Katibu Tawala Msaidizi Mipango na Uratibu amemshukuru Padri Bilingi kwa kutimiza ahadi yake na kwamba atahakikisha kila halmshauri inapata miche ya miti hiyo kama ilivyotarajiwa huku akiahidi kufikisha taarifa hiyo kwa Mhe. Mhandisi Gabriel.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kipekee inatoa shukrani  za dhati kwa Padri Bilingi kwa kuwa kiongozi wa dini anayeenenda kwa mfano kupitia kitendo chake cha kutimiza ahadi aliyoitoa mwenyewe.

“Tukumbuke kuwa, Padri Bilingi amefanya kazi ya utunzaji wa mazingira kwa kugawa miche ya miti mingine tofauti na mikwaju tangu mwaka 1978 alipohudumu katika maeneo mbalimbali yakiwemo Bugando - Mwanza, Musoma, Nyarubele n.k”




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa