• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RAIS SAMIA AMETUPA FARAJA- CCM GEITA

Posted on: August 24th, 2023

Na Boazi Mazigo- Geita RS


Katika hali ya kufurahisha, Kamati ya Siasa ya CCM Mkoa Geita imeeleza kuridhishwa kwake na uboreshwaji wa huduma kwa jamii hususan afya baada ya kupata shuhuda kutoka kwa wananchi.

Hayo yamejiri Agosti 24, 2023 baada ya kamati hiyo kufanya ziara na kujionea utoaji wa huduma kwenye kituo cha afya Katende wilayani chato ambacho hapo awali ilikuwa ni zahanati tangu mwaka 1975 hadi mwaka 2021. Ilipopandishwa hadhi.

Akiongea kwa wakati tofauti, mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni mwenyekiti wa CCM Mkoa Geita Nicholaus Kasendamila alisema," waliosema huduma ni nzuri ni wananchi, hivyo sisi tumpongeze Mhe.Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa namna anavyotupa faraja kuboresha huduma. Lakini pia ajira ziliongezeka kutokana na kupanuliwa kwa huduma na kwa kuboreshwa, wananchi wamepata huduma bora"

Mwenyekiti Kasendamila aliongeza kuwa, ni vyema wahudumu na watumishi kwa ujumla kuendelea kuwatia moyo, kuwahudumia wananchi na kudumisha mahusiano, Upendo na mshikamano na kwamba miradi ya serikali inapokuja ni vyema kupokelewa na kusemewa kwa wananchi.

Kwa upande wake Mganga mkuu halmashauri ya wilaya Chato Dkt. Eugen Rutaisire alisema, "kwa sasa hali ya upatikanaji wa dawa ni asilimia 93 na wakazi wa Katende wanaishukuru sana serikali kwa huduma nzuri inayotolewa na kuahidi mbele ya kamati hiyo kuendelea kutoa huduma stahiki kwa Wananchi"

Vilevile Mwenyekiti wa Kijiji cha Katende Bw.Nzoka Butigu aliihakikishia kamati hiyo kuwa huduma zipatikanazo kituoni hapo ni nzuri na zinawaridhisha kisha kuishukuru serikali.

Pamoja na mradi huo, kamati ilipita na kutembelea miradi inayotekelezwa wilayani hapo ambapo gharama yake yote ni zaidi ya shs. Bilioni 42.3


Kamati hii itaendelea na ziara yake Agosti 25, 2023 katika wilaya ya Geita.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa