• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC Gabriel Afanya Ziara ya Kushtukiza – Agundua Ujanja Unaofanywa na Kampuni ya Uchenjuaji Dhahabu ya Ombeo Group Mjini Geita

Posted on: June 25th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amefanya ziara ya kushtukiza katika kampuni ya Uchenjuaji Madini ya Dhahabu ijulikanayo kama Ombeo Group iliyopo Mtaa wa Nyamalembo Mjini Geita na kujionea namna ambavyo bado wapo wafanyabiashara wanaoendesha shughuli zao bila kufuata taratibu na hivyo kuendelea kutorosha utajiri wa Geita na kuikosesha serikali mapato yake halali kupitia rasilimali Madini ya Dhahabu.

Hayo yamejiri mapema leo tarehe 25.06.2018 majira ya asubuhi, ambapo Mhe. Mhandisi Gabriel aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na Mkoa pamoja na waandishi wa habari ili kushuhudia tukio hilo.

Akiongea baada ya kupita na kuona shughuli zinazofanywa ndani ya eneo hilo ilihali shughuli hizo kuwa zimefungwa na Afisa Madini Mkazi Mkoa wa Geita kwa zaidi ya siku thelathini nyuma, Mhe. Mhandisi Gabriel alisema, “ hapa kama mvayoona kazi zinaendelea na hii ni sehemu tu ndogo ya jinsi ambavyo mali zetu za Nchi zinachukuliwa; Serikali imekuwa ikipigana kulinda rasilimali zetu hizi adimu, Geita hii ni ya Dhahabu, Nchi hii inapambana kuhakikisha Sekta ya Madini inaleta matokeo makubwa katika uchumi wa Nchi, lakini kuna wizi mkubwa unafaywa na wageni kwa mgongo wa wenyeji”. Aliendelea kwa kutoa ONYO kali kwa wote ambao wanaendeleza jitihada za kutorosha Madini ndani ya Mkoa wa Geita na kwamba operesheni ndiyo kwanza imeanza hivyo waache mara moja .

Kwa upande wake Afisa Madini Mkazi Mkoani Geita Bw. Ali Said Ali alieleza kuwa, hapo awali Kampuni hiyo ilipigwa faini ya Shilingi Milioni Tatu na Laki Tano na Baraza la Taifa la Mazingira (NEMC) kutokana na uchafuzi wa mazingira iliyousababisha, pamoja na faini hiyo kutokulipwa hadi sasa, aliwafungia kufanya shughuli za uchenjuaji kwa kuwawekea Lakiri (Seal) mwezi mmoja nyuma mpaka hapo watakapokuwa wamekidhi matakwa ya kisheria ikiwemo kuwa na leseni hivyo naye kusikitishwa na kampuni hiyo kukutwa tena ikiendelea na uzalishaji. Hivyo alikazia kwa kusema, endapo kampuni itakutwa na makosa baada ya uchunguzi kukamilika, faini haitapungua Shilingi Milioni Hamsini na kutaifishwa kwa mali.

Mwisho, Mhe. Mhandisi Gabriel aliviagiza vyombo vya Ulinzi na Usalama kwa kushirikiana na Ofisi ya Madini kufanya uchunguzi ,kujiridhisha kwa siku ya leo  tu juu ya mambo yaliyokiukwa kwa mujibu wa sheria za nchi ili kuweza kuchukua hatua stahiki na kwamba hatamwonea yeyote bali sheria zitafuatwa.

Miongoni mwa waliokutwa ndani ya eneo la Kampuni hiyo ni raia wa kigeni Wachina wane, wanaume watatu na mwanamke mmoja, pamoja na Mtanzania mmoja mwanaume.

Geita ni mahala salama pa mwekezaji kuja kuwekeza akizingatia sheria na taratibu za nchi katika uendeshaji wa shughuli zake. Hivyo ni vyema kwa wafanyabiashara kuhakikisha wanafuata sheria na kulipa kodi stahiki kwa serikali wanapofanya shughuli zao ili kuepuka adhabu mbalimbali zitokanazo na uvunjaji wa sheria mbalimbali za nchi.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa