• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC Gabriel Awaachia Changamoto Watumishi wa Sekta ya Ardhi Geita Kupima Viwanja kwa Tshs. 50,000/=

Posted on: April 4th, 2019

Leo Aprili 04, 2019 , Wataalam wa sekta ya ardhi kutoka halmashauri za mkoa wa Geita wamekutana kwaajili ya kujadili mambo mbalimbali yanayohusu makusanyo ya kodi ya ardhi, upangaji, upimaji na umilikishaji ardhi ndani ya mkoa huu katika ukumbi wa mikutano, ofisi ya mkuu wa mkoa wa geita.

Akiongea wakati wa kufungua kikaokazi hicho, Mkuu wa mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel ameeleza kutoridhishwa na mwenendo wa makusanyo ya kodi ya ardhi ndani ya mkoa huku akilinganisha ukubwa wa ardhi iliyopo na ile iliyopimwa na kuona ni kama vile hakuna ardhi iliyopimwa hivyo kuwaachia wataalam hao changamoto ya kuhakikisha wanakuja na mpango kabambe wa kupima ardhi geita.

Mhandisi Gabriel amewaeleza wataalam hao kuwa, “ jamii ina changamoto, mapato ya wananchi bado ni kidogo, familia zetu bado zina changamoto, ambapo ardhi ilionekana kuipima ni gharama kubwa sana. Pamoja na serikali kutoa maelekezo na bei elekezi kwenye baadhi ya maeneo, naomba niwaache na pendekezo moja kuwa, kwanini msiwatangazie geita upimaji wa eneo kwa shilingi elfu hamsini tu ndani ya mkoa?”.

Wataalamu hao wameendelea kuelezwa kuwa, endapo wananchi watafanikiwa kupimiwa maeneo yao itapunguza kero kubwa, ardhi yao haitakuwa mfu, wataweza kupata mkopo, vitakuwa na thamani vikiuzwa lakini pia mtaepusha migogoro isiyokuwa na sababu ya watu kuingiliana mipaka.

Wito ukatolewa kwa vijana waliohitimu kwa fani ya upimaji na hawana ajira, kujitolea kuichangamkia fursa hiyo endapo pendekezo alilolitoa mhandisi Gabriel litakubalika ukizingatia tayari ofisi za kanda itaazimisha vifaa bure vya kufanyia kazi hiyo endapo vikihitajika, huku akiwataka kuhakikisha wanapangilia vizuri miji yao ili uwepo ukanda wa kijani kila unapoingia katika halmashauri husika.

Kipekee mhandisi Gabriel amekemea tabia ya watumishi wanaoendelea kusababisha migogoro ya ardhi akisisitiza utoaji wa elimu inayohusu masuala ya ardhi ili wananchi waelewe ni kwa kipindi gani watanyang’anywa eneo wasipoyaendeleza ili wawe na uelewa. Vilevile wataalam hao wamekumbushwa juu ya kupeleka kusudio la kuwashitaki wadaiwa wote ambao kwa muda mrefu sasa hawajalipa kodi za ardhi. Mkuu wa mkoa amemaliza kwa kuwasihi wataalam wa ardhi kuhakikisha wanapanga mji, na maeneo ambayo bado hayajaharibiwa ili kuwasaidia wananchi lakini vilevile kutengeneza taswira ya miji na kuifanya ikuwe.

Naye Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Miundombinu Charles Saguda kwaniaba ya watumishi wa sekta ya ardhi wa mkoa wa geita akamshukuru mgeni rasmi na kuahidi kuwa, ombi alilolitoa kwao watalifanyia kazi na kuleta mrejesho huku wakija na mkakati kabambe wa kuendesha zoezi zima la upimaji.

Kikao kazi hicho kimehudhuriwa na watumishi mbalimbali akiwemo Afisa Ardhi Kanda ya Ziwa Nicolas Kawishe,Maafisa Ardhi, Maafisa Mipangomiji, Wathamini, Wapima Ardhi bila kusahau warasimu ramani

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa