• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC Geita Aendeleza Jitihada Uanzishwaji wa Soko la Dhahabu, Akutana na Benki Mbalimbali

Posted on: February 4th, 2019

Ni mwendelezo katika hatua za awali kufanikisha uanzishwaji wa vituo/masoko ya ununuzi wa madini ya dhahabu, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Mhandisi Robert Gabriel amekutana na kufanya mazungumzo na benki ili kuona namna zitakavyoshiriki kufanikisha jambo hili zuri na la kiuchumi.

Katika kikao hicho kilichofanyika tarehe 04.02.2019 kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa wa Geita na kuhudhuriwa na wawakilishi benki za BoT Kanda ya Ziwa, CRDB, NBC, NMB na Azania pamoja na ofisi ya Madini na TRA Mkoa wa Geita, Mhandisi Gabriel amewaeleza wajumbe hao kuwa, lengo kuu ni kuanzisha soko la madini ya dhahabu haraka iwezekanavyo kwa kuzingatia uwepo wa huduma zote zinazohusiana na ufanikishaji biashara hiyo kubwa ya dhahabu.

Amesema, “nimewaita hapa lengo ikiwa ni kuona namna gani taasisi za fedha mnashiriki katika katika uanzishaji wa soko la dhahabu, nini kifanyike ili mwisho waa siku wanunuzi na wauzaji wa dhahabu wamalize mambo yote sehemu moja. Tumeamua kuondokana na hatari ya kubeba fedha nyingi, sasa twende kidijiti (digital) tukae na wateja tuwaeleze madhara ya kubeba fedha nyingi mkononi lakini vilevile tuzuie utakatishaji wa fedha”

Vile vile Mhandisi Gabriel amewapa changamoto TRA na Ofisi ya Madini Mkoa wa Geita kujipanga kuweza kuhudumia wafanya biashara wa madini na kukusanya mapato ya serikali huku utaratibu ukiandaliwa wa kuwakutanisha na kuwaelimisha juu ya namna biashara hiyo itakavyokuwa ikifanyika eneo moja kwenye kituo/soko kuu la mkoa, kisha akawatembeza wajumbe hao kwenye eneo zitakapowekwa taasisi hizo za fedha.

Wakati huo huo, Mhandisi Gabriel amependekeza uundwaji wa mfumo utakaotumika kuratibu biashara hiyo na kwamba kutakuwa na uwezo wa kujua ni kiasi gani cha dhahabu kimepatikana na kimeuzwa kwa siku, cha thamani ipi na mapato ya serikali yamekusanywa kwa kiwango gani, wazo lilipokelewa vyema na kuungwa mkono na BoT wakisema kuwa, wanaamini wataalam wao wa TEHAMA kwa kushirikiana na wa Madini, Halmashauri na TRA wataweza kufanikisha suala hilo na kwamba kama BoT wapo tayari kutoa ushauri kufanikisha jambo hilo.

Kwa upande wao taasisi za fedha wamesema, wapo tayari kuwahudumia wafanyabiashara hao wakisisitiza wananchi kutumia mifumo ya kisasa ya uhamishaji na ulipaji fedha na si kupenda kutembea na fedha taslimu kwani ni hatari kwa usalama wa maisha na wataendelea kuhamasisha suala hilo.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa