• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC Geita Afanya Hamasa Ugawaji Vitambulisho vya Wajasiliamali, Ahimiza Matumizi ya CHF Iliyoboreshwa.

Posted on: March 6th, 2019

Wajasiliamali wadogodogo ni miongoni mwa kundi ambalo Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Mhe .Rais Dkt. John Pombe Magufuli imelipa kipaumbele kwa hukikisha wanaepukana na kero zitokanazo na ushuru/tozo mbalimbali na hivyo kuja na vitambulisho kwaajili yao vinavyouzwa shilingi elfu ishirini kwa matumizi ya mwaka mmoja.

Jitihada hizo zinapelekea uongozi wa mkoa huu kupitia Mkuu wa Mkoa Mhe. Mhandisi. Robert Gabriel kufanya ziara ya kushtukiza tarehe 05.03.2019 katika Soko la Lyobaika, Kijiji cha Lyobaika katika kata ya Uyovu ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe ili kujiridhisha kama wajasiliamali hao wanafanya biashara zao wakiwa na vitambulisho. Baada ya kupita kwa wajasiliamali hao anagundua kuwa, wengi hawakuwa na vitambulisho hivyo akaamua kuitisha kikao cha pamoja ili kuzungumza nao juu ya umuhimu wa vitambulisho hivyo huku akiwahamasisha kuvichangamkia.

Amesema, “tunapenda nyote mpate vitambulisho hivi lengo ikiwa mfanye shughuli zenu bila bugdha yoyote kama lilivyo agizo la Mhe. Rais, lakini mkumbuke kuwa, orodha yenu ni muhimu kuwezesha mipango ya serikali hata katika ujenzi wa masoko".

Baada ya fursa ya maswali na majibu, Mhandisi Gabriel akawapa muda wa hadi tarehe 01.04.2019 kuwa wamemaliza zoezi hilo la kuwa na vitambulisho huku akiwahahakikishia kutotozwa fedha yeyote kwa atakayechukua kitambulisho na kwamba endapo wataombwa fedha baada ya kuwa na utambuzi huo, wasitoe kiasi chochote na atawashughulikia watakaojaribu kufanya hivyo.

Akimaliza kuongea na wananchi hao, Mhandisi Gabriel amewahimiza juu ya matumizi ya Bima ya CHF Iliyoboreshwa ambapo mwananchi ataweza kupata bima hiyo kwa shilingi elfu thelathini huku akitibiwa na wategemezi wake sita, kwamba ni mkombozi wa wao waichangamkie.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mhe. Said Nkumba alimtambulisha Mkuu wa Mkoa kwa wajasiliamali na kuwaambia kuwa, kila mjasiliamali ambaye mtaji wake hauzidi milioni nne anao wajibu wa kuwa na kitambulisho hicho.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Soko hilo, Bw.Gembe Kahindi   amewaomba wajasiliamali hao wasiendelee kuweka visingizio ilihali wamepata auheni ya ulipaji ukizingatia zamani walikuwa wakitozwa ushuru mdogo mdogo ambao kwa mwaka ulifikia hadi shilingi elf sabini, lakini kwa sasa ni kidogo, hivyo kuishukuru serikali kwaniaba ya wajasiliamali waliokusanyika hapo, kisha mkutano kufungwa na kuacha walikuwa hawana vitambulisho hivyo wakivichangamkia.  




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa