• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC Shigela Awahamasisha Walimu Kutumia Benki ya NMB

Posted on: July 14th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe.Martine Shigela ametoa wito kwa walimu wote ndani ya Mkoa wa Geita kutumia huduma zinazotolewa na Benki ya NMB.

Mhe. Shigela ametoa kauli hiyo alipokuwa akifungua Kongamano la Walimu Spesho lililoandaliwa na Benki ya NMB Julai 14,2025 Katika Ukumbi wa Mikutano wa Otonde Manispaa ya Geita.

Mhe.Martine Shigela amesema kuwa NMB ni Benki yenye masharti nafuu kwa utoaji wa mikopo kwa walimu na wateja wao wengine Mkoani Geita. Aidha watumie fursa ya kongamano lililoandaliwa kwani litawasaidia walimu kupata mikopo kwa masharti nafuu ,kupata elimu ya utunzaji wa fedha na kujua fursa za biashara zilizopo mkoani Geita.

              "Program ya mwalimu spesho imetupa mikopo kwa masharti rafiki mpaka walimu wamejenga nyumba za kuishi kwa kigezo cha hati ya kiwanja,pili unapata elimu ya kutunza fedha na inafundisha fursa za kibiashara"ameongeza Mhe.Shigela

Mkuu wa Mkoa wa Geita amewasisitiza walimu wanaofanya biashara kupata elimu kupitia Program hii ya Mwalimu spesho ili kujitoa kwenye janga la umasikini na magonjwa mkoani Geita.

Aidha ameipongeza benki ya NMB kwa kuboresha huduma za kibenki kidigitali ambazo zinamfanya mtumiaji aweze kupata huduma ya kutoa na kutuma pesa wakati wowote na mahali popote pindi akijiunga na mtandao wa kibenki (Internet bank).


Mkurugenzi  wa Manispaa ya Geita Ndg.Yefred Myenzi  ameipongeza benki ya NMB kwa kuboresha huduma za fedha kwa kuangalia walimu ambao ni kiungo kikubwa katika jamii.

Aidha amewasisitiza NMB benki kuwa kipaumbele kuhakikisha wanaikumbuka jamii kwa kutoa madawati mashuleni, vifaa tiba kwenye vituo vya afya pamoja na kuhamasisha watumishi wa umma na wafanyabiashara kutumia huduma ya kidigitali ya Internet bank.

Kwa Upande Wake Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa Bi.Faraja Ng'ingo,amesema Kongamano hili linatimiza miaka 10, lengo mahususi ni kuwahudumia walimu, kukutana na walimu kwa ajili ya kuwaelimisha kuhusu akaunti maalum ya vikundi,maboresho ya mikopo ya "Mshiko fasta"ya kukopa kidigitali mpaka shilingi Milioni kumi.

Aidha ameongeza kuwa Kongamano hili limelenga kutoa elimu kuhusu ujasiriamali,kilimo,biashara,elimu ya fedha,teknolojia,ustaafu na afya.

Kongamano hilo limefanyika Nchi nzima likiongozwa na kauli mbiu isemayo"Mwalimu Spesho,Ushiriki Endelevu Wenye Tija"


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • RC Shigela Awahamasisha Walimu Kutumia Benki ya NMB

    July 14, 2025
  • Dkt. Kijaji Azindua Chanjo ya Mifugo na Uvikwaji Hereni Kwa Ng'ombe Geita

    July 09, 2025
  • Epukeni Tabia ya Utoroshaji Mapato- RAS Geita

    July 01, 2025
  • Bukombe na Mbogwe Zapongezwa Kwa Kupata Hati Safi

    June 23, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa