• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC Tabora Asifu Utendaji wa Mhe.Rais Magufuli, Akubali Somo la RC Geita.

Posted on: March 14th, 2019

Ni siku moja kabla ya kikao cha ujirani mwema kitakachofanyika kuanzia tarehe 15-16.03.2019 katika mkoa mwenyeji Geita. Kipekee tena, ni siku chache kuelekea ufunguzi wa soko la dhahabu Geita utakaofanyika tarehe 17.03.2019, ambapo Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Tabora ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe.Aggrey Mwanri ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa huo inawasili mkoani hapa na kupokelewa na wenyeji wao ambao ni Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Geita.

Baada ya mapokezi hayo, wote wanakutana na kufanya mazungumzo katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita na baada ya neno la ukaribisho, RC Tabora anapata nafasi ya kuzungumza.

Mhe.Mwanri Anasema, “nikushukuru sana kwa ukaribisho. Leo tumekuja kujifunza kuhusu Geita, na kwakutambua hilo, wenzangu inabidi kwanza tukiri kuwa hatujui ili tuweze kujifunza, hivyo sisi wana Tabora tuliona tuje mapema. Tuna hakika tukishajifunza, tutakuwa na badiliko la ghafla la kitabia”

Hakuishia hapo, bali Mhe. Mwanri anaendelea kugusia kuhusu elimu iliyotolewa na RC Geita wakati wa utangulizi akisema, “tumejifunza namna tunavyoweza kupata mapato ya serikali. Lakini tambueni yakuwa mkoa wenu ni wa kipekee na umebarikiwa kutoa kiongozi wa Taifa hili, Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli, tunayempenda sana, anayeitetemesha dunia, hivyo tuige kutoka kwake”

Katika kikao hicho, RC Tabora anamhakikishia RC Geita kuwa, wanakwenda Tabora kutumia ujuzi watakaoupata mkoani hapa, na watakapofanikiwa watahakikisha wanaualika Mkoa wa Geita ukaone matunda ya mafundisho yake kwao, na itakuwa ni mafanikio makubwa, kwani lengo ni kupata mapato yatakayowasaidia kusukuma maendeleo mbele, huku akiendelea kumpongeza kwa kutokuwa mchoyo wa elimu kwakuwa wengine huficha siri ya mafanikio wakiogopa kupitwa kimaendeleo.

Awali akiukaribisha ujumbe huo kutoka Tabora, RC Geita Mhe.Mhandisi.Robert Gabriel ametumia ubao kufafanua mambo mbali mbali akiwaambia wajumbe hao kuwa, “siri kubwa ya ya mafanikio ni kuishirikisha jamii, usimamizi mzuri, kuwa na uongozi bora, bila kusahau maadili na mtandao mwema”

Mhandisi Gabriel amewaeleza pia juu ya namna alivyosimamia fedha zitokanazo na migodi, yani fedha za wajibu wa makampuni kwa jamii (CSR), ambapo kupitia mgodi mmoja wa dhahabu Geita (GGM), miradi mbalimbali imetekelezwa ikiwemo ya elimu na afya pamoja na ile ya kimkakati kama vile vibanda vya soko, uwekaji taa barabarani, pamoja na uandaaji wa eneo la kipekee la uwekezaji, ukanda wa utalii bila kusahau maeneo ya maonesho.

Baada ya kumaliza mazungumzo ofisini, Mhandisi Gabriel anaupeleka ujumbe wa Tabora kushuhudia baadhi ya miradi inayotekelezwa na fedha za CSR ikiwemo vibanda kuzunguka soko kuu, ndani ya Halmashauri ya Mji Geita. Hakika wamejionea na kujifunza mengi.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa