• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

REA Kutoa Mikopo Ujenzi Vituo vya Mafuta Vijijini

Posted on: October 2nd, 2023

Na Lilian Lundo na Veronica Simba

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imekuja na mpango wa kutoa mikopo midogo kwa ajili ya kujenga vituo vya mafuta vidogo vidogo vijijini ili kuzuia ajali za moto zinazotokana na kuuza mafuta ya Petroli kwenye madumu.

Hayo yamesemwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko wakati wa hafla ya uwashaji wa umeme wa REA Jimbo la Geita Mjini, mkoani Geita leo Oktoba 2, 2023.

“Tumekuja na mpango wa kuwapa watu mikopo midogo, tuanzishe vituo vya mafuta vidogo vidogo vijijini ili watu wetu waache kuuza madumu ya Petroli humu, na baadae wanapata ajali ya kuunguzwa na mafuta hayo,” amesema Mhe. Dkt. Biteko.

Vilevile amesema kuwa Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini inagawa mitungi ya gesi kwa ruzuku ndogo ili kuwasaidia Wanawake Watanzania kupika kwa kutumia nishati hiyo mbadala.

“Rais anapenda wanawake Watanzania, ameyaona mateso yao ya kupika kwa kutumia kuni, tumekuja na nishati mbadala ya kuwasaidia Wanawake wa Tanzania wapike kwa kutumia nishati mbadala,” amesema Mhe. Dkt. Biteko.

Wakati huo huo Mhe. Dkt. Biteko amewaomba viongozi wote waliochaguliwa na kuteuliwa kusimamia miradi ya Serikali na fedha zote zinazoletwa ziwahudumie Watanzania.

“Hakuna maana yoyote, sisi viongozi kuwa tunaishi maisha ya mjini lakini wananchi wetu wa vijijini hali zao ngumu. Mhe. Rais anatoa fedha kwa ajili ya watu hawa, anatoa fedha anajima, anapambana kwa ajili ya maendeleo ya watu, anataka kuona wananchi wanahudumiwa,” amesema Mhe. Dkt. Biteko.

Hivyo ametoa wito kwa viongozi wote, kuhudumia wananchi masikini wanaotaka kujipambanua kupata maendeleo yao.

Naye, Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mhandisi Jones Olotu amesema Serikali imetoa shilingi bilioni 39.1 kwa ajili ya kuweka umeme vijiji vyote vya Mkoa wa Geita ambavyo havijpata umeme.

Aidha ametaja miradi mitatu inayoendelea kutekelezwa katika Jimbo la Geita Mjini kuwa ni Mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili, Mradi wa Kupeleka umeme Pembezoni mwa Miji pamoja na Mradi wa Kupeleka umeme kwenye Vituo vya Afya na Pampu za Maji.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa