• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RMO GEITA ASISITIZA IMARISHWAJI AFYA YA UZAZI WA MAMA NA MTOTO.

Posted on: November 2nd, 2023

Na Abraham Mwasimali- RS Geita

Katika kuendeleza jitihada za kuimarisha afya ya uzazi wa mama na mtoto, mganga mkuu Mkoa wa Geita Dkt.Omari Sukari alitoa wito kwa wadau kujadili usalama na namna ya upatikanaji wa bidhaa za afya ya uzazi, mama na mtoto.

Wito huo ulitolewa Novemba 1, 2023 wakati akifungua kikao kazi kujadili masuala yahusuyo afya ya uzazi wa mama na mtoto kilichofanyika kwa siku mbili katika ukumbi wa hoteli ya Alphendo iliyopo mjini Geita.

Akifungua kikao kazi hicho, Dkt.Sukari alisema lengo ni kujadili namna ya kuweka mipango madhubuti ya upatikanaji wa bidhaa za afya ya uzazi, mama na mtoto ili zinapatikane muda wote kwa ajili ya kupunguza vifo vya wajawazito na watoto wachanga lakini pia bidhaa hizo zitawasidia vijana wa rika balehe ambao pia ni wanufaika wa huduma hizo.

‘’tutajadili hasa namna ya upatikanaji wa bidhaa za afya muda wote kwa ajili ya wakina mama wanao toka kujifungua ili kupunguza hali ya vifo kwa watoto wachanga na wajawazito vinavyojitokeza na pia wanufaika wengine ni vijana wetu ambao wapo kwenye rika la kubalehe ambao pia ni wanufaika wa afya ya uzazi kwa vijana’’. Alisema Dkt Sukari

Aidha katika hatua nyingine, Dkt Sukari alisema lengo jingine ni namna ya kuwafikia wananchi kwa ajili ya kujua umuhimu wa matumizi ya uzazi wa mpango kwa njia ya kisasa ili kupunguza vifo vya watoto wachanga pamoja na vifo vya mama wajawazito.

“kwa mujibu wa tafiti ya “Tanzania Demographic and Health Survey and Malaria Indicator” (TDHS-MI), asilimia 22 ya kina mama kati ya umri wa miaka 15 mpaka 49 wanatumia njia za uzazi wa mpango. Hii bado ni asilimia ndogo, hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha tunafikia  asilimia 45 za kutumia matumizi ya kisasa ya uzazi wa mpango kama lilivyo lengo la Taifa. Hali ya vifo vya watoto wachanga vimepungua kutoka 556 mpaka 104 kwa vizazi hai 100,000 kwa Taifa, hivyo ni wajibu wetu  kuhakikisha dawa za dharura zinakuwepo ili kuendelea kupunguza vifo hivyo’’. Aliongeza Dkt.Sukari


Kwa upande wake mjumbe wa kikao hicho bw. Hemedi Mahamudu alisema kuwa, kamati ya kikao hicho itahakikisha kinatoa njia madhubuti katika kuhakikisha huduma za afya ya uzazi wa mama na mtoto zinatolewa kwa wakati wote kwa kuzingatia uwepo wa dawa muhimu kwa kila kituo cha afya, pamoja na kuzisimamia dawa ili ziweze kuwafikia walengwa wa huduma hii  ili kupunguza vifo vya mama wajawazito na watoto.

‘’ndugu wajumbe wa kikao hiki, tunatakiwa tuweze kuimarisha njia mahususi za upatikanaji wa  bidhaa za afya ya uzazi wa mama wajawazito na watoto ili tuweze kupunguza kiwango cha vifo vya kina mama wanaotoka kujifungua, watoto pamoja na vijana walio katika kipindi cha barehe  Pia, ni vyema tuhakikishe tunatoa dawa kwenye vituo vyetu vya kutolea huduma za afya kwa mujibu wa takwimu za wagonjwa tulio nao”. Alimaliza bw. Mahamudu



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa