• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Mamlaka za Serikali za Mitaa
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Sensa ni Kipaumbele Chetu Hadi Agosti 23, 2022”. Asema RC Shigella.

Posted on: August 5th, 2022

Na Boazi Mazigo-Geita

Mkuu wa Mkoa Geita Mhe. Martin Shigella amesema kwa sasa pamoja na shughuli zinazoendelea, kipaumbele cha Serikali ni zoezi linalokuja la Sensa ya Watu na Makazi.

Amesema hayo Agosti 5, 2022 akiwa ofisini kwake punde tu baada ya kulakiwa na viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na wa Chama Tawala CCM pamoja na Sekretarieti ya Mkoa na Watumishi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita.

Akiongea baada ya kupokelewa RC Shigella ameeleza yakuwa, amefarijika kuwa mkoani Geita na anamshukuru Mhe.Rais kwa kumuamini na kumteua kuwatumikia Watanzania wa Geita huku akisema “ninamshukuru sana Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuniamini tena na niwashukuru kwa ukarimu wenu wakati wa mapokezi na niwapongeze kwa kuendelea kufanya kazi kwa bidii kikubwa tushirikiane kuendeleza mazuri ambayo wenzetu waliyafikia na kuboresha zaidi palipo na changamoto”.

Aidha, RC Shigella ameeleza kuwa, “kipaumbele chetu ni kuwatumikia wananchi, tukatatue kero zao, tuwafuate walipo na tusisubiri watufuate maofisini. Tutambue Mhe.Rais ana matarajio mengi na wananchi wanamuamini, hivyo tusimwangushe. Lakini pia pamoja na kazi nyingine, Sensa ya Watu na Makazi ni kipaumbele chetu kwa sasa hadi Agosti 23, hivyo viongozi wote tuhakikishe tunashiriki kikamilifu kuhamasisha wananchi washiriki na tupate taarifa sahihi tuweze kuisaidia serikali kupanga vyema kwa ajili ya maendeleo”.

Mhe.Shigella amemaliza kwa kuhimiza ushirikano miongoni mwa watendaji, wananchi na wadau mbalimbali na kuwakumbusha watendaji kuhakikisha wanaweka juhudi na kuboresha mikakati katika ukusanyaji wa mapato huku akizipongeza Halmashauri zote za Mkoa wa Geita kwa kuvuka lengo la ukusanyaji wa mapato katika mwaka wa fedha 2020/21 na kuipongeza Serikali kwa kuleta fedha nyingi za bajeti zikiongezeka mfululizo kwa miaka mitatu kutoka zaidi ya Bilioni 222.5 kwa mwaka wa fedha 2022/23 hadi zaidi ya Bilioni 288.4 kwa mwaka wa fedha 2022/23.

Mkoa wa Geita ulipata viongozi wapya baada ya uteuzi uliofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Samia Suluhu Hassan Julai 28, 2022 ambapo Mhe.Martin Reuben Shigella aliteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa Geita na Prof.Godius Walter Kahyarara aliteuliwa kuwa Katibu Tawala Mkoa Geita na tayari wamewasili mkoani hapa na kuanza kazi wakati zoezi la makabidhiano lilingojewa.




Matangazo

  • MATOEKEO YA KIDATO CHA SITA YATANGAZWA July 05, 2022
  • HOTUBA YA BAJETI YA NCHI KWA MWAKA WA FEDHA 2022/2023 June 01, 2022
  • BAJETI YA MKOA June 28, 2022
  • Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan Amemuapisha Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Staki Senyamule Tarehe 19 Mei 2021 May 19, 2021
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Ukiuza Toa Risiti, Ukinunua Dai Risiti-Asisitiza RC Shigela

    August 12, 2022
  • RC Shigela Akabidhi Pikipiki 8 CBWSOs Mkoani Geita, Aagiza Zitumike kwa Malengo Kusudiwa.

    August 11, 2022
  • RC na RAS Geita Wajitambulisha kwa Watumishi Wilayani Geita, Wasisitiza Kuinua Uchumi.

    August 11, 2022
  • RC na RAS Geita Wajitambulisha kwa Watumishi Wilayani Geita, Wasisitiza Kuinua Uchumi.

    August 11, 2022
  • Tazama Zote

Video

Mwaliko Jukwaa la Fursa za Biashara Mkoani Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa