• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

Posted on: May 17th, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Martine Shigela amebainisha kuwa Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inajali na kuvithamini vyama vyote vya Ushirika Nchini kwa sababu ni mojawapo ya msingi wa maendeleo ya Taifa.

Mhe. Shigela ametoa kauli hiyo alipokuwa akiongea na wanachama wa vyama vya Ushirika kutoka katika Wilaya zote za Mkoa wa Geita wakati wa Maadhimisho ya Jukwaa la Maendeleo ya Ushirika katika Mkoa wa Geita ambalo limefanyika Mei 16, 2025 katika Ukumbi wa CCM Wilayani Bukombe.

Mhe. Shigela ameeleza kuwa Serikali kupitia wataalam wake imeendelea kutoa elimu juu ya umuhimu wa vyama vya ushirika kwa wanachama mbalimbali, pia iliona changamoto zinazowakabili wana ushirika katika utendaji kazi zao za kila siku ikaanzisha Taasisi ya kifedha kwa ajili ya kuwawezesha wanachama hao kupata mikopo yenye riba nafuu.

“Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshalifanyia kazi suala la mikopo na upatikanaji wa mikopo kupitia Benki ya Ushirika Tanzania, Pia wakulima na wafugaji wameendelea kunufaika na mbegu bora za mazao, madawa ya mifugo pamoja na pembejeo zote za kilimo na mifugo hivyo ndugu zangu wana ushirika hatuna budi kutoa shukrani zetu za dhati kwa Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutuwezesha.” Aliongeza Mhe. Shigela

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Geita ametoa agizo kwa watumishi pamoja na makampuni ambayo yana madeni katika vyama mbalimbali vya ushirika kulipa madeni hayo ili kuwezesha vyama hivyo kuendesha shughuli zao bila mikwamo.

Kwa upande wake Mrajis wa Vyama vya Ushirika Mkoa wa Geita Bi. Doreen Mwanri amebainisha changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta hiyo kuwa ni pamoja na baadhi ya vyama vya ushirika kushindwa kurejesha mikopo kwa wakati na hivyo kuweka malimbikizo ya madeni ambayo huzorotesha maendeleo ya sekta ya Ushirika pamoja na baadhi ya Makampuni ya ununuzi wa mazao ya kilimo kushindwa kulipa ushuru/ tozo mbalimbali kwa vyama vya Ushirika na kusababisha makusanyo ya Serikali kuwa hafifu na kutofikiwa malengo yaliyopangwa.

Mkoa wa Geita una jumla ya Vyama vya Ushirika 600, ambapo vyama 298 vimesajiliwa kwenye mfumo wa MUVU vikiwa na wanachama 25,249. Vyama hivi vimegawanyika katika Sekta mbalimbali za uzalishaji kama vile Kilimo, mifugo, uvuvi, SACCOS na jamii. Maadhimisho ya Jukwaa la Ushirika mwaka 2025 lililongozwa na Kauli Mbiu isemayo “USHIRIKA HUJENGA ULIMWENGU ULIO BORA.”

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Wafanyabiashara Wadogo Wahamasishwa Kujisajili

    May 15, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa