• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Sitaki nione Halmashauri yoyote Tanzania itakayokwenda Kukopa Pesa kwenye Mabenki kwa Ajili ya Mradi wowote katika wilaya zao” JPM

Posted on: November 28th, 2019

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amewaagiza Wakurugenzi wote Nchini kuacha tabia ya kukopa Fedha kwa ajili ya kuzitumia Kwa kutekeleza Miradi ya Maendeleo kwenye maeneo yao. Ameyasema hayo jana Jioni Mjini Ushirombo wakati akiwasalimia wananchi wa Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita alipokua akielekea Wilayani Chato.

Awali akiwasalimia wananchi waliomlaki kwenye Mji wa Masumbwe Wilayani Mbogwe Mhe Rais alimtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo kuhakikisha anajenga Barabara za Lami kwani zinadumu Muda mrefu.

Aidha, aliwataka viongozi Wilayani Mbogwe kuacha kuwa wapole kwani kwa kufanya hivyo wanachelewesha Maendeleo Wilayani humo, ni lazima wakemee uzembe na Kuhakikisha wanabuni Mambo ya Msingi kwa ajili ya Kuinua Wialaya hiyo. “Simamieni Maendeleo ya Wananchi wenu, nataka Barabara za Lami hapa”  alisema JPM.

Akiwa kwenye Mji wa Runzewe alisimama pia kuwasalimia wananchi Lukuki waliokuwa wamejipanga kandonkando ya Barabara kumwona Rais wao na aliwapongeza Wananchi hao kwa kufanya kazi kwa bidii na kubadilisha Mji wa Runzewe na kutunza Mazingira.

Mhe. Rais alitoa pongezi kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi wa Wilaya ya Bukombe aliyejitambulisha kwa jina la Afande Kusura kwa kusimamia vizuri Amani ya wananchi wa Wilaya hiyo kwani sasa hali ni shwari sio kama zamani ambap kulikuwepo na Matukio ya Ujambazi na Uvunjifu wa Amani.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel alimshukuru Mhe Rais kwa kuwaelekeza kuanzisha Masoko ya Dhahabu Nchini kwani yameleta matunda makubwa kwenye Mapato ya Dhahabu ambapo alisema Mapato yatokanayo na Dhahabu iliyopatikana ndani ya miezi 10 ya Mwaka 2019 Mkoani Geita kutoka kwa wachimbaji wadogo ni Asilimia 51 ya Dhahabu yote iliyopatikana kwa miaka yote Mkoani humo kwani zimepatikana Kilo 2522 zenye Thamani ya Bilioni 237 wakati Mwaka 2016 ni Bilioni 23 pekee zilipatikana.

Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Said Nkumba alimshukuru Mhe Rais kwa kuwaletea Timu ya Mawaziri Wanane aliyoituma kwenda kwenye Hifadhi Wilayani humo ambayo ziara yao ilimaliza Kabisa migogoro ya Wakulima na Sehemu za Malisho kwa Wafugaji kutokana na Mapendekeoz waliyayatoa kwake.

Baadae Mhe. Rais aliwasalimia wananchi wa Kijiji cha Nyakayondwa na aliwataka kutunza Mazingira wanapofanya Shughuli za Kilimo kwenye Pori linalowazunguka kwani wakilitunza na kuwapa Manufaa  kwa muda mrefu.

Kwa mapenzi Makubwa kwa Wananchi pamoja na Uchovu wa Safari na Mikutano mingi njiani, Mhe. JPM alisimama tena kwenye kijiji cha Bwanga kuwasalimia Wananchi na aliwasihi wote kuhakikisha Wanachapa kazi ili kujiletea maendeleo yao wenyewe.

Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa