• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TASAF III Yainua Maisha ya Bibi wa Miaka 100, Ashuhudia Mafanikio yake

Posted on: June 26th, 2019

Yawezekana wengi wetu hatufahamu ni kwa jinsi gani Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inawakumbuka wananchi wake kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo inayoitekeleza TASAF ikiwemo.

Kutana na ushuhuda mfupi wa bibi Malosha Shingisha (100), mkazi wa kijiji cha Ibambila, Kata ya Nyang’hwale, Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’hwale Mkoani Geita ambaye ni Mlengwa wa Mpango wa Kunusuru Kaya Masikini (TASAF III) alipotembelewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhandisi Robert Gabriel Juni 25,2019 katika ziara yake kufuatilia maendeleo ya walengwa wa TASAF ndani ya Mkoa huu.

Bibi Malosha anaeleza kuwa, yeye ni miongoni mwa walengwa wanaotoka kwenye kaya masikini na kwamba awali hakuweza kumudu gharama za maisha ikiwemo kushindwa kupata mlo zaidi ya mmoja kutokana na ugumu wa maisha aliyokuwa nao ukilinganisha na sasa.

“naishukuru sana serikali yetu inayoongozwa na Rais Magufuli kupitia mpango huu wa TASAF kwani umeniwezesha sana. Sasa nimejenga nyumba, nimenunua kuku ninafuga, mbuzi saba na kondoo mmoja lakini nasomesha wajukuu watatu na ninalima. Namshukuru sana Rais Magufuli kwa kuendelea kuruhusu fedha hizi kutufikia. Zimebadilisha maisha yangu na familia yangu”,asema bibi Malosha.

Kwa upande wake mhandisi Gabriel ameendelea kushuhudia mabadiliko kwa wananchi wa Geita Walengwa wa Mpango wa TASAF huku akiwapongeza viongozi kuanzia ngazi ya kijiji, kata, halmashauri na mkoa kwa namna wanavyosimamia vyema mpango huo, vilevile kuwataka wataalam kuendelea kutoa mafunzo mbalimbali ili kuwaimarisha zaidi huku akiishukuru serikali ya awamu ya tano kwa jinsi inavyoendelea kuwajali wananchi wake.

Taarifa iliyotolewa na mtendaji wa kijiji hicho bw. Charles Nhungukila inaeleza uwepo wa mpango huo tangu mwaka 2015 una walengwa/kaya 96 ambazo awali zilimudu kupata mlo mmoja kwa siku lakini sasa hupata milo mitatu kwa siku, maisha yao yamebadilika.

Shughuli wanazojishughulisha nazo haswa ni kilimo, ufugaji, uuzaji maziwa, wamejenga nyumba, wanamiliki na kukodi mashamba n.k

Kupitia bibi huyu, jamii inapaswa kuelewa kuwa, mtu haitaji kuwa na fedha nyingi ili kupiga hatua kimaendeleo kwani walengwa wengi hupokea fedha hadi shilingi elfu ishirini kila baada ya mwezi mmoja na huitumia vizuri hadi kuwaletea mabadiliko. Wengi huanza kwa kufuga kuku, kisha zinapoongezeka hubadilisha kwa mbuzi, kisha ng’ombe na kuwawezesha kumiliki ardhi na kujenga pia.

Hivyo basi kwa ushuhuda huu, kila aliyebarikiwa kuwa na nguvu anapaswa kujishughulisha apate kipato ili kuepukana na jamii tegemezi.


Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa