• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TFS Wapongezwa na Mwenge wa Uhuru 2025

Posted on: September 6th, 2025


Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2025 Ndugu Ismail Ali Ussi ametoa pongezi kwa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania kwa kuwa wabunifu kwa kutunza vyanzo vya maji ambavyo vimeleta ahueni kwa wananchi kupata maji kwa ajili ya kunyweshea mifugo pamoja na matumizi mbalimbali ya nyumbani.

Ndg. Ismail Ali Ussi ametoa pongezi hizo tarehe 6 Septemba 2025 Mwenge wa Uhuru ulipotembelea chanzo cha maji mto Mtakuja kilichopo katika Shamba la miti Silayo Kata ya Minkoto Wilayani Chato na kuzindua kampeni ya upandaji miti katika chanzo hicho.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa 2025 ameeleza kuwa TFS wana jukumu la kusimamia uhifadhi wa misitu lakini wamejiongeza na kuwa wabunifu katika kutoa faraja na upendo kwa wananchi wa Kata ya Minkoto na maeneo jirani kwa kutunza vyanzo vya maji.

Akitoa taarifa ya mradi huo kwa niaba ya Mkuu wa shamba la miti Silayo, Bw. Lwamuhoza Elizeus amesema chanzo cha maji mto Mtakuja ni moja kati ya vyanzo vya maji Zaidi ya 14 vilivyopo ndani ya shamba la miti Silayo kikitiririsha maji yake kuelekea Kijiji cha Minkoto.

Bw. Lwamuhoza Elizeus ameongeza kuwa chanzo hicho kilichoanza kufufuliwa na kuzalisha maji kuanzia mwaka wa fedha 2017/2018 kimewanufaisha wananchi takribani 2000 wa vitongoji vya Mtakuja, Usukumani, Mwabasabi na Nyalubere katika kijiji cha Minkoto ambao wanapata maji ya kutosha kwa matumizi ya kila siku kama kunywesha mifugo, kupikia, kufulia na kuendesha shughuli za kilimo cha umwagiliaji kupitia maji yanayotiririka.

“ Baadhi ya faida zilizopatikana kutokana na uwepo wa chanzo hiki ni pamoja na  wananchi wa kijiji cha Minkoto hususan wanawake wamepunguziwa umbali wa kwenda kutafuta maji  kutokana na upatikanaji wa maji ya uhakika, kuchangia uhifadhi wa uoto wa asili, kudumisha mfumo wa ikolojia katika eneo la hifadhi, kusaidia uoteshaji wa miche na ukuzaji wa miti ambayo hutolewa bure kwa wananchi.” Aliongeza Bw. Lwamuhoza Elizeus.

Bw. Lwamuhoza Elizeus ameeleza kuwa mpango endelevu wa TFS ni kuongeza kasi ya uhifadhi wa vyanzo vya maji kwa kupanda miti rafiki kwenye vyanzo vya maji, kutoa elimu ya uhifadhi wa vyanzo vya maji kwa wananchi, kuchukua hatua za haraka juu ya shughuli yoyote inayohatarisha uhai wa vyanzo hivyo vya maji, kuendelea kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Chato katika kutekeleza mikakati endelevu ya utunzaji wa vyanzo vya maji vilivyopo ndani na nje ya hifadhi.










Matangazo

  • MAONESHO YA NANE YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI 2025 August 14, 2025
  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Maendeleo yote Yanaletwa na Walimu- Waziri Mkuu

    October 04, 2025
  • Sekta ya Madini Yapaisha Pato la Taifa- Dkt. Biteko

    September 28, 2025
  • Wadau na Wananchi Geita Waaswa Kuendeleza Sekta ya Madini

    September 25, 2025
  • Fursa Zitolewazo na Serikali Kunufaisha Wajasiriamali Wadogo

    September 23, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa