• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Tuige Mema na Uadilifu wa Watumishi Wenzetu Waliotutoka- Asema Mhe. Senyamule

Posted on: February 20th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe. Rosemary Senyamule Leo Februari 20, 2022 Katika Ukumbi wa GEDECO Uliopo Mjini Geita Amewaongoza Mamia ya Waombolezaji Kutoa Heshima za Mwisho Kwa Miili ya Marehemu Mhandisi Edgar Mungaya na Bw.Magai Mkama, Watumishi wa Wakala wa Barabara za Vijini na Mijini (TARURA) Mkoani Geita Waliofariki kwa Ajali ya Gari Februari 18, 2022  Wilayani Geita.

Akizungumza Kabla ya Kuanza Zoezi la Kutoa Heshima za Mwisho, Mhe. Senyamule Amewaasa Watumishi Kuendelea Kujifunza Uchapakazi na Uadilifu Kama wa Watumishi Hao waliotangulia Mbele ya Haki na Kutoa Wito kwa Madereva Kuzingatia Sheria za Usalama Barabarani Huku Akiwaomba Ndugu, Jamaa na Marafiki wa Familia Kuendelea Kudumu Katika Imani na Kumtegemea Mungu Wakati Wote Kwani Yeye Ndiye Faraja Tosha.

"Nimesikia Wasifu wa Marehemu Wote. Kupoteza Watendaji Mwenye Ujuzi na Utaalam, ni Uchungu Sana Ukizingatia hata Wahandisi ni Wachache. Sisi Kama Binadamu Tuombe Mungu Atufariji, Tuwe na Tumaini kwa Mungu". Alisema Mhe. Senyamule

"Neno la Biblia Linasema, Japokuwa Amekufa Angali Anaishi. Neno Hili Litupatie Tumaini. Vilevile, Niwaombe TARURA Kama Itawapendeza, Wahandisi Muipe Barabara Hata Moja jina la Mhandisi Edgar ili Kuenzi Mchango Wake". Alimaliza Mhe. Senyamule Kisha Kuwatakia Safari Njema Wanaosafiri Kwenda Kuwapumzisha Marehemu

Akitoa Neno la Faraja Wakati wa Shughuli Hiyo, Askofu wa Kanisa TAG Geita Mchungaji Simon Masunga Alisema, "Ni Vyema Tuliobaki Kuilinda Imani ili Tuumalize Mwendo Salama, Kwakuwa Kifo Hakina Taarifa. Lakini Pia Tuendelee Kukemea Roho Mbaya Ambayo Sasa Inashamiri Geita ya Watu Kujinyonga na Kutupa Watoto"

Awali Akitoa Salam za Rambirambi, Katibu Tawala Mkoa wa Geita Bw. Musa Chogero Ametoa Pole Kwa Watumishi na Taasisi ya TARURA Kwa Kuondokewa na Watumishi Wawili Kwa Wakati Mmoja Jambo Ambalo Si Jepesi. Vilevile Ametoa Pole kwa Kanisa na Familia Akisistiza Kuwaombea Marehemu Kila Mtu Kwa Imani Yake Ili Waendelee Kupumzika Kwa Amani.

Marehemu Mungaya Ameacha Mjane na Mtoto Mmoja, na Marehemu Magai Ameacha Mjane na Watoto Watano.

Mwili wa Marehemu Mhandisi Edgar Mungaya Umesafirishwa Kueleka Mkoani Arusha na Mwili wa Marehemu Bw.Magai Mukama Umesafirishwa Kuelekea Mkoani Shinyanga Kupitia Runzewe Bukombe Kwa Ajili ya Maziko.

Bwana Ametoa, na Bwana Ametwaa, Jina Lake Lihimidiwe.


Boazi Mazigo

AFISA HABARI

RS- GEITA



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa