• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

"Tunataka Kutengeneza Kizazi Kijacho Chenye Akili Nyingi”. Asema RC Geita.

Posted on: February 14th, 2022

Mkuu wa mkoa wa Geita Mhe.Rosemary Senyamule ameeleza kusikitishwa kwake kwa namna ambavyo wengi wa maafisa Lishe ndani ya mkoa huo wamekuwa wakitekeleza majukumu yao bila kufikia malengo jambo ambalo limechangia kuurudisha nyuma mkoa katika baadhi ya maeneo kwenye suala la lishe.

Hayo yameelezwa leo Februari 14, 2022 katika ukumbi wa mikutano wa Mwl.Julius Nyerere EPZA-Geita Mjini wakati Mhe.Senyamule akifunga kikao cha Tathmini ya Mkataba wa Lishe Mkoa.

“kwakweli sijafurahishwa na mrejesho kutokana na tuliyoyaazimia kikao kilichopita, hivyo niombe mwende mkayafanyie kazi tuliyokubaliana kwakuwa kama mkoa tunataka kutengeneza kizazi cha watanzania wenye akili ya nyingi ya kutosha kutokana na lishe iliyo bora. Sasa mtambue tu ya kuwa, suala la lishe si ombi, si hiari bali ni wajibu wetu kutekeleza” alisema Mhe.Senyamule.

Vilevile Mhe.Senyamule amewaagiza wakurugenzi kuhakikisha wanatenga fedha ili kuwezesha shughuli za lishe kwenye halmashauri zao ili kufikia malengo, kisha kuipongeza halmashauri ya mji Geita kwa jinsi inavyojitahidi.

Baada ya kumaliza mjadala kuhusu lishe, Mhe.Senyamule amewaagiza wakurugenzi wa halmashauri za mkoa wa Geita kuwawekea malengo maafisa chanjo wao ili waweze kuwasaidia wananchi kwa kuwahimiza kupata chanjo ya kujikinga na ugonjwa wa UVIKO-19, lakini pia kuwahimiza walezi na wazazi kuwapeleka watoto kwenye vituo vya kutolea huduma za afya kwaajili ya kupata chanjo ili kujikinga na magonjwa mbalimbali ikiwemo Surua Rubela.

Awali, Bi.Riziki Mbilinyi ambaye ni Afisa Lishe Mkoa aliwasilisha tarifa ya utekelezaji ambayo ilionesha kuwa bado halmashauri nyingi za mkoa wa Geita hazijafanya vizuri hususan kipengele cha matumizi ya fedha kuwezesha shughuli za lishe.

Naye Afisa Chanjo wa Mkoa Bi.Wille Luhangija alitoa taarifa ya mwenendo wa utoaji wa Chanjo za kawaida kwa watoto na ile ya UVIKO-19 ambapo ilionesha kuwa, mwitikio umekuwa mdogo na kwamba jitihada zaidi zinahitajika kwa ushirikiano wa pamoja ili kuongeza idadi ya wachanjwaji. Vilevile alisisitiza kuwa mkoa unazo chanjo za kutosha aina nne za Sinopharm, Pfizer, Moderna na Johnson Johnson (JJ).Pia Luhangija ameongeza kuwa, mkoa umefanikiwa kuongeza vituo viwili vya chanjo ya UVIKO-19 katika hospitali ya Geita na  Mgodi wa GGML.

Kikao hicho kilihudhuriwa na wakuu wa wilaya, wakurugenzi, sekretarieti ya mkoa, waganga wakuu wilaya, waweka hazina, maafisa mipango na maafisa lishe wa mkoa wa Geita.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa