• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Tupeleke Mafunzo ya Mfumo wa PVMIS Ngazi za Vituo- Asema Dkt.Mkapa

Posted on: March 16th, 2023

Wataalam wa Ununuzi na ugavi, TEHAMA, famasia pamoja na waganga wakuu kutoka halmashauri zote za mkoa wa Geita wamepewa wito kuhakikisha mafunzo waliyopewa juu ya utekelezaji mfumo wa kielektroniki wa usimamizi wa taarifa za Mshitiri (Prime Vendor Management Information System) yanazifikia timu zilizopo ngazi ya vituo ili kuleta ufanisi pale mfumo utakapoanza kutumika.

Wito huo umetolewa na mganga mkuu halmashauri ya wilaya Bukombe dkt.Deograsia Mkapa kwaniaba ya mganga mkuu mkoa Geita wakati akiahirisha mafunzo hayo Machi 16, 2023 katika ukumbi wa mikutano halmashauri ya mji Geita na kuhimiza washiriki kwenda kuanzisha na kusimamia timu ngazi za vituo ili kutokukwamisha matumizi ya mfumo huo pale utakapoanza kufanya kazi.

“kwanza niwapongeze wakufunzi mmetufundisha kwa vitendo, lakini washiriki wenzangu niwapongeze kwa umakini na niombe sasa twendeni tukasimamie uundwaji wa timu ngazi za vituo lakini pia tujipange kufundisha ndani ya muda mfupi kutoka sasa tusichukue mda mrefu ili mfumo huu usijesahaulika”, alisema dkt.Mkapa.

Dkt.Mkapa amemaliza kwa kuiomba OR-TAMISEMI kushughulikia maoni yaliyotolewa na wajumbe katika kuboresha mfumo ili unapoanza angalau mawazo yao yawe yamefanyiwa kazi kwa lengo la kuongeza ufanisi.

Kwa upande wake bw.Amiri Mhando ambaye ni mjumbe wa kitaifa wa kamati ya uratibu ya Prime Vendor System (PVS) alisema, wanaishukuru ofisi ya mkuu wa mkoa kupitia katibu tawala mkoa kwa kufanikisha uendeshaji mafunzo hayo kupitia wakurugenzi kuwaruhusu wataalam hao kuja kupokea mafunzo na maelekezo juu ya mfumo. Ameshauri pia uundwaji wa kamati ufanyike lakini shughuli za matumizi ya mfumo zifate sheria, taratibu na kanuni, hivyo visingizio havitarajiwi kwenye matumizi ya mfumo huu.

Mwisho, bw.Mhando alisema ni muhimu kuzingatia utoaji wa taarifa ngazi ya mkoa pale ambapo washiriki hao watatarajia kutoa mafunzo.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa