• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Tushikamane Kwakuwa Mradi wa Jengo la Mama na Mtoto ni Wetu Sote”. Asema Dkt. Shekalage

Posted on: February 24th, 2022

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Seif Shekalage ameeleza kufurahishwa kwake kwa jinsi ziara aliyoifanya ilivyozaa matunda kwa kutatua kwa pamoja changamoto iliyokuwa ikichelewesha kuanza kwa ujenzi wa Jengo la Mama na Mtoto (Maternity Block) tangu mwaka 2021 katika hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita.

Hayo yameelezwa Februari 23, 2022 katika ukumbi mdogo wa mikutano kwenye ofisi ya mkuu wa mkoa wa Geita wakati wa kikao kazi kutafuta utatuzi wa changamoto zilizokwamisha Ujenzi wa Jengo la Mama na Mtoto.

Akiongea wakati wa kuhitimisha kikao kazi hicho, Dkt. Shekalage amempongeza Katibu Tawala Mkoa wa Geita Bw. Musa Chogero ambaye ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa kikao kufuatia utendaji wenye kuleta matokeo, huku akihimiza uwazi, uzalendo, mawasiliano na mshikamano kwa wajumbe wakati wote mradi huo utakapoanza kutekelezwa ili kuwatendea haki wananchi wa Geita , Mhe.Rais na Wizara kwa ujumla kwani huduma hiyo ni muhimu sana.

“hongereni Geita kwa kumpata kiongozi huyu msikivu, ni mtu wa matokeo ndiyo maana wizara imemuamini. Lakini pia, niwaombe timu hii kuwa binafsi sitaki kuwa sehemu ya kufeli, kwahiyo tushikamane kwa pamoja ili mradi huu uanze kutelezwa mara moja na kuanzia tarehe 30 Machi, 2022 mkandarasi awe ameingia kazini”. Alisema Dkt. Shekalage.

Aliendelea kusema, “pamoja na hayo, bila mawasiliano yaliyojengeka vizuri hatutaweza kufanikisha utekelezwaji wa mradi huo. Hivyobasi tuwe wamoja, kwani mradi huu ni wetu sote, na mwisho tunatakiwa kutoa matokeo ya kitu kimoja, jengo la mama na mtoto”.

Awali, Katibu Tawala Mkoa wa Geita Bw.Musa Chogero alimueleza Naibu Katibu Mkuu huyo kuwa, mkoa umejiandaa kwenda na kasi kwenye utekelezaji wa mradi huo kwani ni hitaji kubwa la wananchi na ni vyema kuwa na matokeo ya haraka na kuwashauri wajumbe wa kikao hicho hususan wataalam kutoa mawazo ambayo yangeweza kutatua changamoto zozote ambazo zingeweza kujitokeza kutokana na aina ya utekelezwaji mradi iliyopendekezwa.

Kikao hicho kilowahusisha wataalam kutoka Wizara ya Afya na kwa  Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wakiwa kama wateja na wawezeshaji, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita kupitia Katibu Tawala wa Mkoa kama msimamizi mkuu wa mradi wote, na Kampuni ya Crystal Consultants kama Mshauri Elekezi .

Kabla ya kikao kuanza, wajumbe wa kikao kazi hicho walizuru kwenye eneo la Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Geita na kuona majengo mbalimbali kisha kuona eneo litakapojengwa Jengo la Mama na Mtoto pamoja na kushuhudia uchimbaji wa msingi wa majengo ya Dharura (EMD) na la Wagonjwa Mahututi (ICU).

Geita ya Dhahabu, Utajiri na Heshima.


Boazi Mazigo

Afisa Habari

Geita RS




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa