• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Ujembe wa Geita Wapokelewa TanTrade, Maandalizi ya Maonesho Makubwa Yaja, Yajayo Yatashangaza

Posted on: November 8th, 2018

Yaliyojiri kwenye kikao kazi kati ya TanTrade na viongozi wa Mkoa wa Geita tarehe 7 Novemba, 2018 katika ukumbi wa mkutano wa TanTrade

Bw Edwin Rutageruka, Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade aliongoza kikao kazi kwa kuwakaribisha viongozi wa Mkoa wa Geita na kusema kuwa, anashukuru uongozi mzima wa Mkoa wa Geita kwa ushirikiano na TanTrade katika kutekeleza majukumu mbalimbali.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Geita Mhe.Mhandisi Robert Gabriel alitembelea Maonesho ya pili ya Bidhaa za Viwanda vya Tanzania mwaka 2017 na Maonesho ya 42 ya Kimataifa ya Biashara kwa lengo la kuona namna TanTrade inavyoratibu Maonesho  na baada ya Ziara hiyo, Mkoa wa Geita kwa kushirikiana na TanTrade waliweza kuandaa Maonesho ya Kwanza ya Teknolojia na Uwekezaji katika sekta ya madini Geita-2018

Mkoa wa Geita mbali na madini na uvivi kwenye eneo la kilimo una fursa nyingi katika mazao ya Alizeti, Asali, Mchele na 'Chia Seeds', Pamba n.k

TanTrade kwa kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Chato iliweza kuwajengea uwezo wazalishaji 106 wa mafuta ya mbegu ya awengine ikiwa lengo la mafunzo hayo ni kuwaunganisha wazalishaji kupata masoko endelevu na TanTrade itahakikisha mafuta ya alizeti yanayozalishwa wilaya ya Chato yanapata 'brand' na kupenya masoko ya ndani na pia itahakikisha mazao hayo yanapata masoko ya nje pia

Nae Ndg Denis Bandisa, Katibu Tawala Mkoa wa Geita amesema kuwa wanaishukuru TanTrade kwa kutoa ueledi wao katika kuandaa Maonesho ya Kwanza ya Teknolojia na Uwekezaji wa Madini- 2018 na tayari Mkoa wa Geita umeshaaza maandalizi ya Maonesho ya pili yanayotarajiwa kufanyika mwaka 2019. Ameongeza kusema kuwa, Mkoa wa Geita unaandaa mradi mkubwa wa ujenzi wa Kituo cha Biashara ambapo ndani ya kituo hicho kutakuwa na eneo la Uwanja wa Maonesho na Eneo la Uwekezaji kwaajili ya Viwanda

Aidha Mkoa wa Geita umeiomba TanTrade iweze kuwasaidia kutoa miongozo katika hatua zote za maandalizi ya mradi huu maana ndio taasisi pekee yenye Mamlaka ya Kudhibiti Maonesho nchini

Pia Mhe.Mhandisi Mtemi Msafiri Simeone, Mkuu wa Wilaya ya Chato alisisitiza kwa kusema kuwa Mkoa wa Geita unania ya kuanzisha mapema Mradi huu mkubwa

Kwa upande wake Bw. Edwin Rutageruka, Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade alihitimisha kwa kusema kuwa “TanTrade itashirikiana na Mkoa wa Geita katika kufanikisha mradi huo na mwaka 2019 itashirikiana na Mkoa wa Geita katika kuratibu Maonesho Teknolojia na Uwekezaji wa Madini mkoani hapo”

Kikao kazi hicho kilihudhuriwa na Ndg Denis Bandisa-Katibu Tawala Mkoa wa Geita, Mhe Mhandisi Mtemi Simeone-Mkuu wa Wilaya ya chato, Mhe Josephat Maganga-Mkuu wa Wilaya ya Geita, Wakurugenzi kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Geita na Geita Mji pamoja na watendaji wengine kutoka Mkoa wa Geita na TanTrade

Imeandaliwa na Kitengo cha Mawasiliano-TanTrade




Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Wafanyakazi Geita Wapewa Rai Kuboresha Taarifa Zao

    May 02, 2025
  • Waziri Mavunde Aaagiza Utekelezaji Wa Miradi Ya Nyuma Ya CSR Geita

    April 15, 2025
  • Mabonanza ya Watumishi Yawe Endelevu - DC Kingalame

    March 30, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa