• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Ujenzi Wa Madaraja Nyang'hwale Kukwamua Wananchi

Posted on: October 4th, 2024


Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2024 zimetoa nuru ya  matumaini kwa wananchi wa Wilaya ya Nyang’hwale baada ya kuweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Boksi kalavati linalojengwa katika barabara ya kutoka Kharumwa hadi Nyijundu.

Akizungumza wakati wa uwekaji wa jiwe hilo la msingi, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2024 Ndugu Godfrey Eliakimu Mnzava amesema kuwa ujenzi wa madaraja mawili katika barabara hiyo utaondoa adha ya usafiri kwa watu na usafirishaji wa mazao na mizigo mingine hususan wakati wa kipindi cha mvua.

Ndg. Mnzava amesema dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha wananchi wake wanapata urahisi wa huduma za usafiri katika kipindi kizima cha mwaka, ndio sababu ya kutoa fedha nyingi kwa ajili ya ujenzi wa madaraja hayo.

Mbunge wa Jimbo la Nyang’hwale Mhe. Hussein Kassu ametoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwakumbuka wananchi ambao kwa takribani miaka 40 wamekuwa wakipata tabu ya kutovuka kutoka upande mmoja hadi mwingine kutokana na kujaa kwa mto Bukungu na kusababisha shughuli za kiuchumi kwa wakulima, wafugaji na shughuli nyingine kukwama.

Ukiwa wilayani Nyang’hwale Mwenge wa Uhuru 2024 umekimbia umbali wa kilomita 137 na kukagua, kutembelea, kuzindua na kuweka mawe ya msingi katika miradi 13 yenye gharama ya shilingi Bilioni tano, ambapo moja ya mradi mkubwa uliozinduliwa ni mradi wa usambazaji umeme katika kitongoji cha Nyamalapa kwa lengo la kuwawezesha wachimbaji wadogo na wa kati wenye viwanda vidogo vinavyojishughulisha na uchenjuaji madini ya dhahabu kufanya kazi zao kwa ufanisi mkubwa.



Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa