• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe za Watumishi |
Geita Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Geita

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
      • Mikakati
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Usimamizi, Ufuatiliaji na Ukaguzi
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Huduma za Maji
      • Miundombinu
      • Elimu
      • Viwanda, Biashara na Uwekezaji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • TEHAMA
      • Mkanguzi Wa Ndani
      • Ugavi na Manunuzi
      • Sheria
      • Mawasiliano Serikalini
  • Wilaya
    • Geita
    • Bukombe
    • Chato
    • Mbogwe
    • Nyang'hwale
  • Halmashauri
    • Halamashauri ya Wilaya Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
    • Halmashauri ya Mji Geita
    • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
    • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
      • Hifadhi ya Taifa ya Rubondo
    • Uchimbaji wa Madini
    • Ufugaji
    • Ufugaji wa Nyuki
    • Kilimo
    • Maeneo ya Viwanda
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Kilimo
    • Huduma Ufugaji
    • Huduma za Uvuvi
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu
    • Mkataba wa Huduma Kwa Mteja
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wadau Wasisitizwa Kuhamasisha Zoezi la Uboreshaji Daftari

Posted on: July 24th, 2024

Wadau Waagizwa Kuhamasisha Zoezi la Uboreshaji Daftari

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Mhe. Jaji wa Rufaa Jacobs C.M. Mwambegele amewaasa wadau mbalimbali wa Uchaguzi katika Mkoa wa Geita kuhakikisha wanashirikiana na Tume kuwahamasisha wananchi wenye sifa ya kujiandikisha kuwa wapiga kura wanajitokeza kwa wingi katika zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura linalotaraji kuanza tarehe 05/8-11/08/2024 katika Mkoa wa Geita.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Uchaguzi ametoa kauli hiyo tarehe 24/7/2024 wakati wa kikao cha wadau mbalimbali wa Uchaguzi kujadili maandalizi ya zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga kura kilichofanyika katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa eneo la Magogo Geita mjini.


Mhe. Jaji Mwambegele ameongeza kuwa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ina matumaini kuwa wadau waliopata fursa ya kushiriki katika mkutano huo watakuwa mabalozi wazuri wa kusambaza taarifa na kuhamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kujiandikisha  na kuboresha taarifa zao ili zoezi lifanyike kwa ufanisi na mafanikio makubwa.

“Katika kuhakikisha tunaenda sambamba na mabadiliko ya Teknolojia, Tume imerahisisha zoezi la uboreshaji wa Daftari ambapo kwa mara ya kwanza mfumo wa uandikishaji utamwezesha mpiga kura aliyepo kwenye Daftari kuanzisha mchakato wa kuboresha taarifa zake au kuhama kituo kwa kutumia aina zote za simu au kompyuta.” Aliongeza Mhe. Jaji Mwambegele.

Mkurugenzi wa Tume Huru ya Uchaguzi Ndg. Ramadhani Kailima amesema kuwa Mkoa wa Geita una vituo 1,637 vitakavyotumika katika zoezi la uboreshaji kwa mwaka huu ikiwa ni ongezeko la vituo 68 katika vituo 1,569 vilivyotumika kwenye uboreshaji wa mwaka 2019/20. Kadhalika Tume inatarajia kuandikisha wapiga kura wapya 299,672 ikiwa ni ongezeko la asilimia 24.7 ya wapiga kura 1,212,146 waliopo kwenye daftari la kudumu la wapiga kura.

Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lillizinduliwa tarehe 20 Julai 2024 katika Mkoa wa Kigoma, Mgeni rasmi alikuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa( MB) ambapo kwa sasa zoezi liko katika mzunguko wa pili wa uboreshaji unaojumuisha Mkoa wa Geita na Kagera.

Zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura kwa mwaka 2024/25 linaongozwa na Kauli mbiu isemayo``Kujiandikisha kuwa Mpiga Kura ni Msingi wa Uchaguzi Bora.”







Matangazo

  • KANUNI MPYA ZA CSR ZA 2023 August 12, 2023
  • Tazama Zote

Habari Mpya

  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Wapatieni Wananchi Taarifa Sahihi za Miradi ya Maendeleo- Msigwa

    May 26, 2025
  • Mkoa wa Geita Kinara Utekelezaji wa Miradi ya TASAF

    May 27, 2025
  • Serikali Inathamini Vyama vya Ushirika- RC Shigela

    May 17, 2025
  • Tazama Zote

Video

Sekta ya Elimu Yazidi Kuimarika Geita
Video Zaidi

Muunganiko wa Haraka

  • Halmashauri ya Wilaya Bukombe
  • Halmashauri ya Mji Geita
  • Halmashauri ya Wilaya Geita
  • Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe
  • Halmashauri ya Wilaya ya Chato
  • Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'hwale
  • E-VIBALI

Tovuti Zinazohusiana

  • IKULU
  • OR-TAMISEMI
  • Utumishi
  • NECTA
  • NACTE
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Maeneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita

    Sanduku la Barua: S.L.P 315

    Simu: 028 2520035

    Mobile: 028 2520035

    barua pepe: ras.geita@tamisemi.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • MMM
    • Ramani ya Tovuti
    • Huduma

Hakimiliki©2017Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita. Haki zote zimehifadhiwa